TRA

TRA

Saturday, July 15, 2017

Uturuki yawaachisha kazi 7000 waliohusishwa na mapinduzi

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



 Rais Reccep Tayyip Erdogan

Serikali ya Uturuki imewaachisha kazi zaidi ya maafisa 7,000 wa polisi, maafisa wa Serikali na wasomi waliokuwa na uhusiano na jaribio la mapinduzi la mwaka uliopita.

Hatua hii imechukuliwa wakati wa kuadhimisha mwaka wa kwanza tangu jaribiio hilo la mapinduzi kuangamizwa.

Zaidi ya watu 250 waliuawa kabla ya jaribio hilo kuzimwa na wanajeshi walioa waaminifu kwa Serikali.

Hatua hii ni sehemu moja tu ya kuwaondoa watu wasio waaminifu ambapo kufikia sasa zaidi ya watu 200,000 wameachishwa kazi.

Rais Erdogan anawalaumu kwa kuunga mkono wapangaji wa mapinduzi hayo yanayodaiwa kupangwa na kiongozi wa kidini aliye uhamishoni Marekani, Fethullah Gulen.

Bwana Gullen anasema kuwa Rais anasema uongo kuhusiana jaribio na mapinduzi hayo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger