TRA

TRA

Tuesday, July 18, 2017

NDEGE YA MAKAMU WA RAIS YAZUILIWA KUTUA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


 Jenerali Abdul Rashid Dostun aijiunga na serikali ya muungano ya Afghanistan

Makamu wa rais wa Afghanistan Abdul Rashid Dostun alijaribu kurudi nchini humo baada ya kusafiri kuelekea Uturuki lakini ndege yake ikakatazwa kutua nchini humo kulingana na maofisa.

Haijulikani ni nani aliyekataza kutua kwa ndege hiyo lakini duru karibu na rais Ashraf Ghani ziliambia BBC kwamba kurudi kwake hakukupangwa na serikali.

Jenerali Dostun aliondoka nchini Uturuki mnamo mwezi Mei huku kukiwa na madai kwamba aliwaagiza watu wake kumteka, kumpiga na hata kumbaka mpinzani wake wa kisiasa.
Amekana kufanya makosa yoyote.

Msemaji wake anasema kuwa alielekea Uturuki kwa ukaguzi wa afya yake.

Atta Mohammad Noor , ambaye ni gavana wa kaskazini mwa mkoa wa Balkh ,alikuwa akisubiri katika uwanja wa ndege wa Mazar-e Sharrif kumpokea Jenerali Dostun siku ya Jumatatu usiku, kulingana na chombo cha habari cha Pajhwok.

Zaidi ya watu 1000 waliandamana na gavana huyo kumpokea mpiganaji huyo wa zamani katika mpaka huo ambao uko karibu na mkoa wa nyumbani wa Jowzjan.

Mashahidi wanasema kuwa baadhi ya wafuasi wa Dostun walikuwa na mabango yaliosema karibu nyumbani kiongozi wetu, kulingana na chombo cha habari cha Reuters.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger