TRA

TRA

Saturday, July 15, 2017

PRODUCER WA RAMA DEE AFURAHI RAMA DEE KUMALIZA BIFU LAKE NA CLOUDS MEDIA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mtayarishaji wa muziki Elly da Bway ambaye amekuwa akifanya kazi kwa ukaribu na Rama Dee amefunguka baada ya msanii wake kumaliza ugomvi wake na kituo cha Clouds.
Akiongea na Bongo5, producer huyo amesema kuwa kitendo hicho kimemfurahisha na kimeleta amani kwake kutokana na kukosa dili la kufanya kazi na wasanii wengine kutokana na ugomvi huo.
Watu wengi walikuwa hawaelewi hii ishu ilivyotokea, walikuwa wakisikia nafanya kazi na Rama Dee moja kwa moja bila hata kufatilia kitu chochote wanakuwa wananijumuisha mimi kwenye mgogoro huo pamoja na studio yangu ninayofanyia kazi. Niliumia sana kwa kuwa hilo liliwafanya wasanii wengi wawe waoga kuja kufanya kazi katika studio zetu mpaka ikafika wakati nikaanza kumshawishi Rama aweze kuweka mambo sawa ilimradi tu niweze kufanya kazi na kila msanii,” amesema Elly.
“Napenda kuwa shukuru Clouds pamoja na maneno yote yaliowahiu kuongelewa lakini walisupport kazi zangu zote nilizotengeneza na hata wimbo wangu mpya wa ‘Boss’ ambao nimeuachia mwezi uliopita umekuwa ukipewa nafasi kubwa kwenye kituo hicho na vituo vingine tofauti tofauti hapa nchini,” ameongeza.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger