Msanii
wa muziki, Q Boy Msafi ameanza maandalizi ya tour yake ya kimaitafa
ikiwa ni miezi kadhaa toka aingie rasmi kwenye muziki akitokea kwenye
masuala ya fashion.
Muimbaji
huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Karorero’, hivi karibuni alikuwa
kwenye BBM Tour ya Young Dee iliyoandaliwa na King Cash pamoja na Mabula
Entertainment, amesema tour hiyo imeweza kumzalishia show mbalimbali.
“Kusema
kweli namshukuru sana Mungu mambo yanaenda vizuri sana, tour ya BBM
imezaa matunda sana, wadau wengi wananipigia simu kutaka show kwahiyo
kwangu naona huu ni mwanzo mzuri wa muziki wangu na kwenda mbali zaidi,”
alisema Q Boy.
Aliongeza,
“Tayari kuna show za kimataifa zimeanza kuja, ni nyingi na mungu
akipenda zitakuwa nyingi zaidi kwa sababu bado kuna watu nazungumza nao
kuhusu show. Lakini yote kwa yote naomba ushirikiano kwa mashabiki wangu
ambao walikuwa na mimi kwa muda mrefu, wadau wa muziki pamoja na
wasanii wenzangu,”
Muimbaji
huyo ambaye alikuwa stylish ya Diamond, aliachana na Kazi hiyo na
kuamua kufanya muziki kwa kuwa ndio plan yake ya muda mrefu.
SHARE
No comments:
Post a Comment