TRA

TRA

Monday, July 17, 2017

Q BOY MSAFI APATA SHAVU HILI LA SHOW ZA KIMATAIFA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Msanii wa muziki, Q Boy Msafi ameanza maandalizi ya tour yake ya kimaitafa ikiwa ni miezi kadhaa toka aingie rasmi kwenye muziki akitokea kwenye masuala ya fashion.
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Karorero’, hivi karibuni alikuwa kwenye BBM Tour ya Young Dee iliyoandaliwa na King Cash pamoja na Mabula Entertainment, amesema tour hiyo imeweza kumzalishia show mbalimbali.
“Kusema kweli namshukuru sana Mungu mambo yanaenda vizuri sana, tour ya BBM imezaa matunda sana, wadau wengi wananipigia simu kutaka show kwahiyo kwangu naona huu ni mwanzo mzuri wa muziki wangu na kwenda mbali zaidi,” alisema Q Boy.
Aliongeza, “Tayari kuna show za kimataifa zimeanza kuja, ni nyingi na mungu akipenda zitakuwa nyingi zaidi kwa sababu bado kuna watu nazungumza nao kuhusu show. Lakini yote kwa yote naomba ushirikiano kwa mashabiki wangu ambao walikuwa na mimi kwa muda mrefu, wadau wa muziki pamoja na wasanii wenzangu,”
Muimbaji huyo ambaye alikuwa stylish ya Diamond, aliachana na Kazi hiyo na kuamua kufanya muziki kwa kuwa ndio plan yake ya muda mrefu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger