TRA

TRA

Monday, July 17, 2017

USIKOSE UZINDUZI WA ALBAMU YA JERUSALEM CITY SINGERS MWANZA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
Uzinduzi wa albamu ya tatu kutoka kwaya ya JERUSALEM CITY SINGERS ya Bugarika Jijini Mwanza, unatarajiwa kufanyika Jumapili ijayo Julai 23,2017 katika viunga vya Rock/ Kishimba Beach Garden Jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa kwaya hiyo, Samwel Maneno amesema hakuna kiingilio katika uzinduzi huo na kwamba shughuli nzima itaanza majira ya saa saba kamili mchana ambapo waimbaji mbalimbali wakiwemo Born To Praise, Voice Of Calvary na Lake Zone watahudumu siku hiyo.
“Hii ni albamu yetu ya tatu ya video iitwayo MUNGU WA AJABU ambapo imetanguliwa na albamu mbili ambazo ni DUNIA MAHUTUTI na HAJAKUSAHAU hivyo nawakaribisha watu wote kushiriki nasi kwenye uzinduzi huo”. Amesema Maneno.
Usikose uzinduzi huu, ni Jumapili ijayo Julai 23,2017 katika viunga vya Rock/ Kishimba Beach Garden Jijini Mwanza, kuanzia saa saba kamili mchana, ambapo hakuna kiingilio. Wasiliana na Jerusalem City Singers 0758 06 10 44
Bonyeza HAPA taarifa zaidi

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger