TRA

TRA

Saturday, July 15, 2017

Walimu waombwa kuisaidia NMB kutoa elimu kibenki

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Profesa Eleuther Mwageni akizungumza na walimu alipomwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kufungua semina ya walimu Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Profesa Eleuther Mwageni akizungumza na walimu alipomwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kufungua semina ya walimu Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB.
Kaimu Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wakati NMB, Abdulmagid Nsekela akizungumza na walimu katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Bi. Vicky Bishubo akizungumza katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Kaimu Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wakati NMB, Abdulmagid Nsekela akizungumza na walimu katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Baadhi ya walimu wakiwa katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Profesa Eleuther Mwageni (kulia) akiondoka ukumbini pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wakati NMB, Abdulmagid Nsekela mara baada ya kufungua semina ya walimu Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB.
WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imewashauri walimu kuisaidia Benki ya NMB kutoa elimu ya masuala ya kibenki na hasa umuhimu wa kujiwekea akiba kwa jamii wakiwemo watoto ili iweze kuwasaidia hapo baadaye. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Profesa Eleuther Mwageni alipokuwa akimwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kufungua semina ya walimu Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB.
Akizungumza kabla ya kufungua semina hiyo, Prof. Mwageni alisema mpaka sasa idadi ya wananchi wanaotumia huduma za kibenki haizidi asilimia 20 jambo ambalo linaonesha bado kuna idadi kubwa ya Watanzania hawatumii mfumo rasmi wa kibenki licha ya manufaa mbalimbali yanayopatikana kwa watumiaji.
Aliipongeza Benki ya NMB kwa hivi sasa kuwa na programu ya kuzunguka mashuleni kutoa elimu za kibenki kwa wanafunzi na wazazi wao na kuonesha manufaa ya kujiwekea akiba kwa wazazi na wanafunzi, hivyo kuwataka waalimu kushirikiana katika kueneza elimu hiyo zaidi kwa jamii nzima. “Hadi sasa si zaidi ya asilimia 20 ya Watanzania wanaotumia huduma rasmi za kibenki…hivyo kuna haja ya kuwaunga mkono NMB kuendelea kutoa elimu za kibenki ili idadi ya watumiaji huduma hizo iongezeke,”
“Nawapongeza pia kwa huduma nzuri za kibenki mnazozitoa kwa walimu, mikopo mbalimbali imekuwa msaada mkubwa kwa walimu pamoja na familia zao…naomba sasa ongezeni na kuwapa mikopo ya kujiendeleza kielimu. Elimu kwao itakuwa msaada mkubwa kwani sasa kuna ushindani wa kila kitu,” alisema Profesa Eleuther Mwageni.
Akizungumza awali kabla ya mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wakati NMB, Abdulmagid Nsekela alisema walimu ni wateja muhimu wa NMB na wametoka mbali na benki hiyo hivyo wataendelea kuwajali kwa kutoa huduma ya kipekee kwao. Alisema wanatambua pia ni watu muhimu katika taifa na jamii kwa ujumla, hivyo kitendo cha kukutana nao kwenye semina hiyo watatoa maoni ambayo yataboresha zaidi benki hiyo.
Alisema NMB itaendelea kuboresha huduma zake kiteknolojia ili kumrahisishia mteja kupata huduma hizo muda wowote na popote. Aliongeza kuwa benki hiyo ni ya kwanza kuja na huduma za simu za kibenki ambazo zimewarahisishia wateja kujihudumia wenyewe kwa baadhi ya huduma. alibainisha hivi karibuni ilileta huduma za NMB wakala ambayo pia imeendelea kuboresha huduma kwa wateja.
Katika semina hiyo iliyowakutanisha walimu wa shule za msingi, sekondari na baadhi ya vyuo na wataalam anuai wa NMB, washiriki watapata fursa ya mafunzo ya kibenki na kutoa maoni mbalimbali yatakayopokelewa na kwenda kufanyiwa kazi lengo ikiwa kuboresha zaidi huduma za wateja wa benki hiyo.
Baadhi ya walimu wakiwa katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Baadhi ya walimu wakiwa katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Baadhi ya walimu wakiwa katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.
Baadhi ya walimu wakiwa katika semina ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na Benki ya NMB. Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni ‘NMB na Walimu Daima’.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger