Ni
kawaida kwa baadhi ya wanawake hasa mastaa kupiga picha wakati wa
ujauzito kwa ajili ya kumbukumbu zao na wakati mwingine kutokana na
mapenzi waliyonayo kupiga picha ambapo mastaa mbalimbali wa kike duniani
wamekuwa wakifanya hivyo.
Jambo
hilo pia tumekuwa tukilishuhudia hata hapa Tanzania na baadhi ya mastaa
pia wameshawahii kupiga picha za namna hiyo na wakati mwingine kuziweka
kwenye mitandao ya kijamii jambo ambalo baadhi ya watu linawakera.
Wema
Sepetu ni mmoja wa watu ambao wameonesha kukerwa na kitendo hicho
akisema ni ukiukwajii wa maadili ya kiafrika na watanzania kwa ujumla na
kuutumia ukurasa wake wa Instagram kumpongeza muigizaji wa Bongomovie
Esha Buheti baada ya kupiga picha akiwa mjamzito ndani ya mavazi ya
kumsitiri.
Wema
ameongeza kwa kusema kuwa ameshakubaliana na hali yake ya kutoweza
kupata mtoto lakini hiyo haimzuii kusema yanayomkera kuhusiana na mambo
ya uzazi.
SHARE
No comments:
Post a Comment