Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema kuwa Iran inajenga viwanda nchini Syria na Lebanon ili kutengeneza makombora.
Majeshi ya Iran yanamsaidia rais Bashar al Assad katika vita vya Syria huku ikiliunga mkono kundi la wapiganaji wa Lebanon Hezbollah.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa Iran inatengeza kiwanda nchini Syria na Lebanon ili kutengeza makombora.
Matamshi ya Netanyahu yanajiri baada ya kufanya mazungumzo na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Gutierrez mjini Jerusalem.
- Israel yaishtumu Iran kwa kujaribu kombora lake
- Iran yawaruhusu wamarekani kuingia nchini mwake
- Marekani yaiwekea Iran vikwazo
- Kwa nini Trump ana msimamo mkali dhidi ya Iran?
- Iran yajaribu kombora la nyuklia
Bwana Netanyahu hakutoa maelezo kuhusu viwanda hivyo vya Iran lakini akaonya kwamba hicho ''ni kitendo ambacho Israel haitakubali''.
Wiki mbili zilizopita, kampuni ya Israel Imgesat ilichapisha picha ilizosema zinathibitisha ripoti ya gazeti moja la upinzani nchini Syria kwamba kiwanda cha makombora kilikuwa kikijengwa kaskazini magharibi mwa Syria chini ya uangalizi wa Iran.
Hakujakuwa na tamko lolote kutoka kwa Iran inayotaka taifa hilo Wayahudi kuangamizwa.
Bwana Netanyahu pia alimshinikiza Guterrez kuhusu walinda amani wa UN nchini Lebanon ,Unifil , ambapo Israel inadai wameshindwa kuwazuia wapiganaji wa Hezbollah kujiongezea silaha tangu vita vya 2006.
Bwana Guterres aliahidi kufanya kila awezalo ili kuhakikisha kuwa Unifil inaafikia malengo yake .
Ninaelewa wasiwasi wa kiusalama wa Israel na narejelea kwamba wazo hilo ama lengo la kuangamiza Israel ni swala ambalo halitakubalika kwa maoni yango.
Mkataba wa Unifil unatarajiwa kuongezwa mwisho wa mwezi.
CHANZO:BBC
SHARE









No comments:
Post a Comment