TRA

TRA

Tuesday, August 29, 2017

NIC Bank Yakabidhi Magari Matatu Kwa Mteja

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Meneja mahusiano kwa wateja wakubwa wa benki ya NIC Tanzania, Woinde Murro (kulia) akizungumza jambo na mmoja wa wateja waliofika kwaajili ya kukabidhiwa magari makubwa ikiwa awamu ya kwanza ya mkopo wa Magari Sita ambapo amepokea magari matatu na matela matatu

Meneja mahusiano kwa wateja wakubwa wa benki ya NIC Tanzania, Woinde Murro(kulia) akimkabidhi funguo  Mkurugenzi wa kampuni ya Usafirishaji ya Simera, Bw.Zainul Dossa(kushoto) za magari matatu waliyokopeshwa na Benki ya NIC
Meneja Uendeshaji kutoka Kampuni ya Usafirishaji ya Simera, Bw. Arif akiwasha moja ya gari mara baada ya Benki ya NIC kukopesha magari sita kwenye kampuni ya Usafirishaji ya Simera jijini Dar es Salaam.
Magari matatu kati ya sita yalikabidhiwa na benki ya NIC kama mkopo kwa mteja wao

Jana benki ya NIC imekabidhi magari makubwa matatu na matela yake kati ya magari sita ambayo yamekabidhiwa kama mkopo kwa Mteja wao Simera. Makabidhiano ya Magari hayo yamefanyika katika Ofisi za FAW zilizopo Barabara ya Nyerere jijini Dar Es Salaam.

Mkurugenzi wa kampuni ya Usafirishaji ya Simera, Bw.Zainul Dossa amepokea magari hayo kati ya sita waliyokopeshwa na Benki ya NIC mapema jana huku magari mengine matatu yatakabidhiwa hivi karibuni.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger