TRA

TRA

Saturday, August 5, 2017

Korea Kaskazini yarusha tena kombora

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

 


Ndege moja ya Ufaransa iliyokuwa na abiria 330 ilikuwa kilomita 100 pekee na kombora la masafa marefu lililorushwa na Korea Kaskazini, maofisa wanasema.

Ndege hiyo ilipita katika eneo ambalo kombora hilo lilinguka dakika 10 baadaye .

Kampuni ya Airfrance inasema kuwa ndege yake haikuwa hatarini lakini imejiweke marufuku ya kusafiri katika anga ya Korea Kaskazini kama tahadhari.

Pentagon inasema kuwa kombora hilo lilipaa katika anga yenye shughuli nyingi.

 Kombora la Korea Kaskazini lilikaribia ndege ya Ufaransa

Maafisa wa Marekani nara kwa mara wamekuwa wakionya kuhusu hatari zinazoletwa na makombora dhidi ya ndege za abiria katika eneo hilo. 

Njia iliotumiwa na ndege hiyo aina ya Boeing 777 inaonyesha kuwa ilikuwa magharibi, mwa Hokkaido, kaskazini mwa taifa la Japan , wakati bora hilo la Korea Kaskazini lilikuwa hewani.

Japan na Marekani inakadiria kwamba kombora hilo lilianguaka kati ya kilomita 100na 150 karibu na ndege hiyo.

"Kombora hilo liliruka katika anga na kuanguka nchini Japan, eneo ambalo hutumika na vyombo vya kibiashara na vile vya uvuvi,"alisema msemaji wa Pentagon Jeff Davis.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger