
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani (kulia) akifafanua jambo wakati
akizungumza na Mtangazaji wa AzamTv, Nurdin Selemani kupitia kipindi cha
Mizani ya Wiki kilichorushwa jana Jumapili.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhani (kushoto)akizungumza na
Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media, Tido Mhando baada ya kushirikia kwenye
kipindi cha Mizani ya Wiki kinachorushwa na Azam Tv Jumapili usiku.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhani (kushoto) ,akimkabidhi
Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Tido Mhando Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa
Mwaka 2015 na Taarifa ya TathminiBaada ya Uchaguzi huo.
Picha na Hussein Makame.
……………………….
Na Mwandishi Maalum
MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhan amevitaka vyombo vya habari
vya Tanzania viige mfano wa wenzao wa Kenya kwa kutumia muda mwingi
kutoa elimu ya mpiga kura.
Akizungumza kwenye kipindi cha
Mizani ya Wiki kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha AZAM Jumapili
usiku, Ramadhan alisema moja ya mambo aliyojifunza katika Uchaguzi Mkuu
wa Kenya ni jinsivyombo vya habari vilivyoshiriki katika Uchaguzi huona
kuchangia watu wengikujitokezakupigakura..
“Natamaninasisivyombo vya
hapanyumbaniviigewenzao wa Kenya ambao walitoa muda mwingi kwa kutoa elimu ya mpiga kura,” alisema Ramadhani.
Bw. Ramadhani aliongeza kuwa
baadhi ya mambo ambayo amejifunzakwa Tume Huru na Mipaka ya Kenya (IEBC)
katika uchaguzimkuuuliomalizikahivikaribuni ni usambazaji wa vifaa
katika vituo vya kupigia kura.
Alifafanua kuwa licha ya kuwa
Kenya wana vituo vichachetakribani 40,000 vya kupigiakuraukilinganisha
na vya Tanzania ambako kuna vituo 65,000, lakini alisema walifanya vizuri
kwenye kusambaza vifaa.
Eneo lingine ambalo lilimvutia ni
namna wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi katika Kituo cha
kupigia kura wanavyokuwa na uelewa mkubwa kuhusu taratibu za kupiga kura.
Kuhusu kuruhusu wafungwa naWatanzania walioko nje kupigakura, Ramadhan alisema kwa sasa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi hairuhusu jambo
hilo na akaongeza kuwa Tume
haina pingamizi iwapo wabunge watatunga sheria inayoruhusu makundi hayo
kujiandikisha na baadaye kupiga kura.
“Tume ya Uchaguzi hainamamlaka ya kuamuaninaniapigekura, ilatunaongozwa na katiba pamoja na sheria,” alisema.
Akizungumza utaratibu wa kupiga kura uliotumika
Kenya, Ramadhani alisema ni mzuri lakini akaongeza kuwa
utaratibu unaotumiwa na NEC uko wazi ukilinganisha na
IEBC.
“Utaratibu wetu ni mzuri zaidi kwani
unatoa fursa ya
mawakala kujiridhisha kwamba mtu aliyeenda kupiga kura ndiye mwenyewe,
unapunguzakelele,” alisema.
Akilinganisha teknolojia iliyotumiwa
na IEBC,
Ramadhan alisema inawezesha mtu akipiga kura inahesabiwa jambo ambalo ilisababisha
IEBC kutangaza matokeo ya awali ambayo hayajathibitishwa na akaongeza
kuwa hilo ni jambo la hatari kwa kuwa matokeo ya
pili yakibadilisha matokeo ya awali inaweza kuleta sintofahamu.
Alisisitizakwambamfumo ambao
unatumiwana NEC badopia ni mzuri kwa kuwa unalengakutangazamatokeo
ambayo yameshathibitishwa na yanaleta amani kwa jamii.
“Uchaguzi ulipitatulitangazamatokeo ya urais ndani ya saa 72 kwa hiyo tuliwahi kuliko wenzetu wa Kenya.”
SHARE
No comments:
Post a Comment