TRA

TRA

Wednesday, August 9, 2017

Vurugu Kenya: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya Wafuasi wa Raila Odinga

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Jeshi la Polisi katika Mji wa Kisumu, nchini Kenya limelazimika kuanza kutumia nguvu kuwatawanya kundi la vijana waliojitokeza mtaani kuanza kuchoma matairi ya magari, wakidai kuibiwa kura kwa mgombea wao wa urais anayeungwa mkono na Muungano wa Nasa, Raila Odinga.

Tukio hilo limetokea baada ya saa chache Odinga kujitokeza mbele ya vyombo vya habari akituhumu uchakachuaji wa kura zake uliofanywa na Tume ya Uchaguzi isiyokuwa na mipaka (IEBC) wakati wa tukio la kuhesabu kura.

Wananchi nchini Kenya walipiga kura katika Uchaguzi Mkuu siku ya jana ,kabla ya vituo hiyo kufungwa kuanzia saa 11:00 jioni.

Polisi walilazimika kutumia nguvu huku wakirusha risasi hewani ili kuwatawanya.

Baadaye Polisi iliamua kuondoa mawe yaliyokuwa yametegwa na vijana hao barabarani.

Katika hatua nyingine, kuna taarifa za kupigana kwa wafuasi wa wagombea ubunge katika kituo vha kujumlishia matokeo , kilichopo Mji wa Mokewe, uliopo Lamu kabla ya Polisi kuwasili eneo la tukio na kurejesha hali ya utulivu

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger