Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, DODOMA
Serikali imepanga kuwasilisha Bungeni mapendekezo ya
Marekebisho ya Sheria za Hifadhi ya Jamii yatakayoanzisha Fao la Upotevu
wa Ajira kwa wafanyakazi watakaokuwa wanapoteza ajira kabla ya
kufikisha umri wa kustaafu kazi.
Akizungumza katika kikao cha Tano cha Bunge la 11, Naibu
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Antony Mavunde amesema Serikali inatambua
changamoto ya wingi wa mifuko inayoikabili Sekta ya Hifadhi ya Jamii
hivyo ili kukabiliana na changamoto hiyo mwaka 2015 Serikali ilifanya
tathamini ya mifuko yote ya Pensheni kwa lengo la kuangalia uwezekano na
namna bora ya
kuiunganisha.
“Matokeo ya tathimini iliyofanyika mwaka 2015 yalionesha
kuwa inawezekana kuunganisha mifuko hiyo na kubaki na michache kwa
kuzingatia hali halisi ya mahitaji”. Alisema Mavunde.
Aidha, Mhe. Mavunde aliongeza kuwa Serikali imeandaa mapendekezo ya kuunganisha
Mifuko mitano inayotoa mafao ya pensheni na kubaki na michache iliyo imara.
Kwa mujibu wa Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) wa
mwaka 1952 fao la kujitoa sio miongoni mwa mafao yalioainishwa katika
mkataba huo.
SHARE
No comments:
Post a Comment