TRA

TRA

Friday, September 15, 2017

Mechi ya Arsenal yakumbwa na ghasia

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Mechi ya Arsenal dhidi ya Cologne katiika kombe la Yuropa ilikumbwa na ghasia na kusababisha kucheleweshwa kwa saa moja.

Maelfu ya mashabiki wa kigeni waliwasili katika uwanja huo bila tiketi na kulikuwa na ghasia kati ya mashabiki na wapokezi wao ndani ya uwanja huo baada ya mlango kufunguliwa.

Maafisa wa polisi walisema kuwa watu watano walikamatwa kwa tuhuma kuhusika katika ghasia.

Mashabiki wa klabu ya Cologne wakiingia katika uwanja wa Emirates
Kulikuwa hakuna ripoti zozote za ghasia wakati wa mechi hiyo ambayo Arsenal ilishinda 3-1.
Timu hiyo ya Ujerumani ilikuwa imepewa tiketi 2,900 pekee.
Lakini takriban mashabiki 20,000 wa timu hiyo waliingia na kusimamisha biashara mjini London nyakati za mchana Alhamisi.
Hatahivyo hivyo mechi hiyo ilianza baada ya kucheleweshwa kwa saa moja.

CHANZO:BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger