TRA

TRA

Monday, May 30, 2016

Magazeti ya Leo

No comments:


 

MISS TANZANIA USA AEESHA KAMARA ATEMBELEA, KUONGEA NA KUTOA MSAADA KENTON HIGH SCHOOL

No comments:


Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara akiongea na wanafunzi wa Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam siku alipotembelea shuleni hapo katika moja ya majukumu yake ya kuhudumia jumuiya. Miss Kamara anadhamini wanafunzi wawili shuleni hapo
Miss Tanzania USA Pageant Aeesha Kamara akimkabidhi msaada mwalimu mipira siku alipotembela shule ya Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania USA Aesha Kamara akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wawili anaowadhamini kwa kuwasomesha shuleni hapo.
Picha ya pamoja. (P.T)

MAHAKAMA KUU KUANZISHWA KATIKA MKOA WA MARA

No comments:


 
Na Lydia Churi- Musoma
Mahakama ya Tanzania inakusudia kuanzisha Mahakama Kuu katika mkoa wa Mara ambapo ujenzi wa jengo la mahakama hiyo unatarajiwa kuanza wakati wowote mwaka huu.
Akizungumza leo mjini Musoma katika ziara yake ya ukaguzi wa shughuli za kimahakama katika kanda ya Mwanza, Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman alisema mkoa wa Mara unayo haki ya kuwa na Mahakama Kuu kwa kuwa nia ya Mahakama ni kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi.
Alisema mahakama hiyo itajengwa kwa haraka na itamalizika katika kipindi cha mwaka moja kwa kuwa fedha kwa ajili ya ujenzi huo tayari imeshatengwa ambapo nyingine imetokana na msaada waliopewa kutoka Benki ya Dunia.
Alisema kuanzishwa kwa mahakama hiyo katika Mkoa wa Mara kutawapa fursa wananchi wa Mara ya kupata huduma kwa karibu zaidi na pia itasaidia kupunguza kesi zilizoko mahakamani kwa haraka.
Awali akimkaribisha Jaji Mkuu ofisini kwake alipomtembelea, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo alimwomba Jaji Mkuu kuanzisha Mahakama Kuu katika mkoa wake kwa kuwa asilimia 55 ya kesi zote za mauaji katika Mahakama kuu kanda ya Mwanza zinatoka katika mkoa wa Mara hivyo mkoa huo unayo haki ya kuwa na Mahakama Kuu.
Pamoja na mkoa huo kuwa na kesi nyingi za mauaji, Mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa wa Mara pia unakabiliwa na kesi nyingi zinazohusu masuala ya ardhi kwa kuwa ni asilimia 38.3 tu ya eneo zima la mkoa huo ndiyo eneo linalotuwa kwa ajili ya makazi ya watu na shughuli za maendeleo
Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, Mkoa wa Mara una wakazi zaidi ya milioni 1.3.
Alisema Mkoa wa Mara una eneo lenye kilometa za mraba 30,150 ambapo asilimia 36 ya eneo hilo ni maji wakati asilimia 25.7 ni eneo lenye mapori na hifadhi za Taifa ikiwemo mbugaya wanyama ya Serengeti.
Aidha, Mkuu huyo wa mkoa aliisifu Mahakama ya Tanzania kwa kufanya kazi yake kwa weledi ya kuzimaliza kesi zilizohusu mapigano ya koo zilizokuwepo katika siku za nyuma mkoani humo kwa kuwa zimesaidia maeneo ya mkoa huo kuwa salama hivi sasa na hayaonyeshi dalili za kujirudia. Aliongeza kuwa eneo la haki likitulia hata masuala ya utawala yakuwa rahisi.
Jaji mkuu Leo amehitimisaha ziara yake katika kanda ya Mwanza yenye mikoa ya Mara, Geita na Mwanza ambapo alikuwa akikagua shughuli mbalimbali za kimahakama katika kanda hiyo.(P.T)

MAANDALIZI YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI TANZANIA 2016/2017 YAANZA RASMI

No comments:


CHU1
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa akihojiwa na waandishi wa habari katika mkutano wa wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Utafiti huo utafanyika nchi nzima kuanzia mwezi Agosti, 2016.
CHU2
Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Fatuma Mrisho akielezea umuhimu wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 katika mkutano wa wadau wa utafiti huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Utafiti huo utafanyika nchi nzima kuanzia mwezi Agosti, 2016.
CHU3
Mkurugenzi Mkazi wa ICAP Tanzania Dkt. Fernando Morales akizungumza katika Mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Utafiti huo utafanyika nchi nzima kuanzia mwezi Agosti, 2016.(P.T)

NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA ZIARANI MKOANI MANYARA

No comments:


Naibu Katibu Mkuu wa CCM,-Bara, Rajab Luhwavi akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Manyara, Luccas Ole Mukusu, alipowasili kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo, mjini Babati, leo Mei 30, 2016. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa huo Ndegesu Ndekobali. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM,-Bara, Rajab Luhwavi akisalimiana na baadhi ya watumishi wa CCM mkoa wa Manyara, alipowasili kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo, mjini Babati, leo Mei 30, 2016. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa huo Ndegesu Ndekobali. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akisaini Kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM mkoa wa Manyara, baada ya kuwasili mjini Babati leo Mei 30, 2016. Kushoto ni Katibu wa CCM wa mkoa huo, Ndegesu Ndekobali. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akisaini Kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM mkoa wa Manyara, baada ya kuwasili mjini Babati leo Mei 30, 2016. Kushoto ni Katibu wa CCM wa mkoa huo, Ndegesu Ndekobali. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi (kulia) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Manyara Joel Bendera alipoenda ofisini kwa mkuu huyo wa mkoa, mjini Babati leo Mei 30, 2016. Kushoto ni Afisa Tawala wa mkoa huo, Eliakim Maswi. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi (kulia) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Manyara Joel Bendera alipoenda ofisini kwa mkuu huyo wa mkoa, mjini Babati leo Mei 30, 2016. 
Katibu wa CCM wa mkoa wa Manyara Ndekobali akishukuru baada ya mazungumzo hayo 
wakiagana baada ya mazungumzo.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akiagana na Afisa Tawala wa mkoa wa Manyara Eliakim Maswi baada ya mazungumzo na mkuu wa mkoa huo Joel Bendera (Katikati), alipoenda ofisini kwa mkuu huyo wa mkoa, mjini Babati leo Mei 30, 2016.
AKAGUA JENGO LA OFISI YA CCM LILILOUNGUA MWEZI MACHI MWAKA HUU 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi (kulia) apata maelezo kutoka kwa Katibu wa CCM mkoa wa Manyara, Ndegesu Ndekobali, alipokagua athari za kuungua jengo la CCM mkoa huo, lililopo mjini Babati. Jengo hilo liliungua Machi 7 mwaka huu. 
Luhwavi akimaliza kukagua jengo hilo.
Baadhi ya viongozi wa CCM wakimkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajabu Luhwavi kuzungumza nao leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM mkoa wa Manyara mjini Babati 
Luhwavi akiingia ukumbini.
Luhwavi akiwa tayari ukumbini.
Katibu wa CCM wa mkoa wa Manyara, Ndekobali akitoa neno la utangulizi.
Baadhi ya watunishi wa CCM kutoka wilaya za mkoa wa Manyara wakimsikiliza Luhwavi.
Masoud Mbengua kutoka Kitengo cha Usalama na Maadili, Makao Makuu ya CCM akizungumza kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Manyara akimkaribisha Luhwavi kuzungumza 
Baadhi ya wafanyakazi wakichukua dondoo, wakati Luhwavi akizungumza nao. (Picha zote na Bashir Nkoromo.

MILLION 100 NA TUSKER FANYA KWELI UWINI YAZINDULIWA NDANI YA KANDA YA ZIWA

No comments:


Kikundi cha TYT kikitoa burudani wakati uzinduzi wa promosheni ya Million 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini kanda ya ziwa uliofanyika jijini Mwanza -Cross Park Bar Igoma.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa wakicheza kufurahia uzinduzi wa Tusker Fanya Kweli Uwini jijini Mwanza.
Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa Patrick Kisaka akitoa maelezo ya promosheni hiyo kabla ya kuzindua rasmi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa promosheni ya Million 100 na tusker Fanya Kweli Uwini, iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza.

Baada ya kutikisa jiji la Dar es Salaam na manispaa ya Moshi leo Kampuni ya Bia ya Serengeti imeendelea kuwapa raha wateja wake kwa kuzindua promosheni ya Milioni 100 na Tusker- Fanya Kweli na Uwini Kanda ya ziwa ambapo Millioni 100 za Tusker Lager kushindaniwa. 

Uzinduzi huo uliofanyika jijini Mwanza Katika Bar ya Cross Park iliyopo Igoma wilayani Ilemela, ulipambwa na maonyesho ya barabarani ambapo msafara ulianzia Kiwanda cha Serengeti Igoma na kuishia Cross Pack Bar huku ukipokelewa na shamrashamra za aina mbalimbali.

 Promosheni hiyo itawapa fursa wateja kujishindia pesa taslimu Milioni 1 kwa washindi kumi (10) kila wiki kwa muda wa wiki kumi na kufanya jumla ya Milioni mia kushindaniwa na Zawadi za bia kibao. Promosheni hii ilizinduliwa rasmi na itaendeshwa kwa muda wa wiki kumi. Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wa Kampuni hiyo pamoja na wana habari.

 Hii si mara ya kwanza kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti kuendesha promosheni kama hii kwani ni wengi wameshanufaika kupitia promosheni mbalimbali za mfumo huu na hata kubadili maisha ya watumiaji wa bidhaa zake kwa kiasi kikubwa. Kupitia bia ya Tusker Lager Kampuni hiyo inaendeleza kile kilichokuwepo cha kurudisha fadhila na kutoa shukrani kwa watumiaji wa bia ya Tusker Lager.                  

Wateja wanaweza kujaribu mara nyingi kadiri wawezavyo. Ili kuwa mshindi wa Tusker milionea, washiriki wataingizwa moja kwa moja kwenye droo kutokana na vocha walizojaza mahali walipopatiwa huduma na wataweza kujishindia pesa taslimu na droo hizo zitachezeshwa kila wiki. 

Mtumiaji anapofungua bia ya Tusker Lager (500ml) chini ya kizibo anaweza kupata kizibo cha ‘Tusker Milionea’ hii itamuingiza katika droo ya kupata Milioni moja, au anaweza kupata ‘Bia ya Bure’ – hii inampa mteja bia ya Tusker papo hapo alipohudumiwa na ikiwa atapata ‘Jaribu tena’ utaendelea kuburudika kistaarabu ili kuongeza nafasi yako kuibuka mshindi. Promosheni hii itasimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini ili kuleta ufanisi zaidi.

Akiongea wakati wa uzinduzi huo jijini Mwanza Meneja Mauzo wa Kanda ya ziwa wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Patrick Kisaka, aliwashukuru wageni wote kwa kuja kuwaunga mkono na kusema kuwa uzinduzi wa promosheni hiyo  ni muendelezo wa kile kilichoanza wiki mbili zilizopita ikiwa ni kutoa shukrani kwa wateja wao kwa kusapoti bidhaa zao.

Alisema “kuendesha promosheni hii ni kurudisha shukrani kwa wajeta wetu kwa kutuunga mkono na kusapoti bidhaa zetu, ambapo tunampa mteja sehemu ya faida tuliyopata Katika mauzo yetu hivyo kuwapa wateja wetu wigo mpana wa kujiinua kimaisha. Kupitia bia yetu ya Tusker Lager tunampa fursa mnywaji na mdau wa bia hii kufanya kweli hivyo watumiaji wa bia ya Tusker wanaweza kujishindia shilingi Millioni moja kwa washindi kumi kwa muda wa wiki kumi ambao tutawapata kutokana na droo tutakazochezesha kila wiki.”

Naye ‘Commercial Planning & Activations Manager’ wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Denis Tairo alisema “Kanda ya ziwa ni sehemu muhimu sana kwa soko letu, wadau wa jiji hili la Mwanza mmekua mstari wa mbele na haikua rahisi sisi kufika hapa leo bila ninyi wadau wetu basi nasi tunasema burudika na bia ya Tusker ili upate nafasi ya kushiriki katika promosheni hii, haijalishi upo wapi na unafanya nini lakini amini kuwa kila wiki ni Millioni kumi zinatolewa kwa watumiaji kumi wa bia ya Tusker.”

Wapenzi na wadau wa Tusker wataweza kushuhudia droo za Promosheni ya Milioni 100 na Tusker zitakazofanyika kila wiki siku ya ijumaa na kurushwa moja kwa moja katika runinga.  Washindi watakaopatikana watakabidhiwa pesa zao ambazo watazipokea kwa njia ya mtandao kila ijumaa inayofuatia kwenye hafla maalum ya makabidhiano. Milioni 100 na Tusker Fanya kweli na Uwini itadumu kwa muda wa wiki kumi nchi nzima. 
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger