TRA

TRA

Wednesday, August 31, 2016

Magazeti ya Leo Alhamisi

No comments:


Read more...

RC ARUSHA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA DINI

No comments:


1
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mheshimiwa Mrisho Gambo(katikati)akizungumza na Askofu wa Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto)  alipomtembelea ofisini kwake 

Askofu wa Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mh.Mrisho Gambo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mheshimiwa Mrisho Gambo akiagana na Askofu wa Kanisa la Anglikan Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kulia)  baada ya mazungumzo yao.
Nteghenjwa Hosseah – Arusha
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo ameendelea  na  ziara yake ya kujitambulisha kwa viongozi wa dini  ukiwa ni utaratibu aliojiwekea wa kukutana na viongozi  baada ya kuteuliwa kushika  wadhifa huo hivi karibuni.
Mh.Gambo amekutana na  Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Mchungaji  Solomon Masangwa , Askofu wa  Kanisa la Evangelistic Assemblies of God(EAGT) mkoa wa Arusha,Leonard Mwizarubi  na Askofu  Stanley Hotay wa Kanisa la Anglikana , Dayosisi ya Mount
Kilimanjaro.
Katika mazungumzo na viongozi hao kwa nyakati tofauti mbali na kujitambulisha aliwahakikisha dhamira ya serikali kulinda na kuheshimu uhuru na haki ya kuabudu ambayo imekuwepo nchini kwa muda mrefu ikiwa ni njia ya kuwa na taifa la watu wenye hofu ya Mungu.
Alisema kutokana na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Joseph Magufuli kutaka kuwainua wananchi wa chini kupitia mapato ya ndani  halmashauri zimetenga asilimia 10 kutoka kwenye mapato hayo kwa ajili ya  mikopo yenye riba nafuu kwa Wanawake na Vijana wajasiriamali  zitakazowawezesha kufanya  shughuli za uzalishaji mali.
Amewataka wawajulishe waumini wa dini zote na serikali iko tayarikupanga utaratibu wa maafisa maendeleo ya Jamii na Vijana kupita na kutoa  elimu kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na madhehebu ya dini hili iwe inufaishe watu wote katika mkoa huu bila kujali itikadi za kidini wala kisiasa.
Askofu Stanley Hotay aliupongeza uongozi wa mkoa kuimarisha hali ya utulivu na kuomba vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo Mkuu wa mkoa ndiye Mwenyekiti wake kukabiliana na changamoto za kiusalama na viashiria vya uvunjifu wa amani.
Aidha alishauri kutokana na idadi ya watu wanaotumia usafiri wa anga kuongezeka kuna haja ya Serikali kufikiria uwezekano wa kupanua zaidi uwanja wa ndege wa Arusha uliopo Kisongo ili uweze kukidhi mahitaji ya sasa badala ya kutegemea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) pekee.
Mh. Gambo amewahakikishia viongozi hao kuwa serikali itakua ikiwashirikisha mipango mbalimbali inayokusudia kuitekeleza ili  watoe mawazo yao katika kuiboresha na  kuifanya itekelezeke   kwa wepesi zaidi.(P.T)

Merkel : Makosa yalifanyika katika suala la wakimbizi

No comments:


 
Kansela Angela Merkel wa Ujerumani amekiri kumefanyika makosa Ujerumani na Umoja wa Ulaya katika suala la mzozo wa wakimbizi lakini amesisitiza kwamba Ujerumani haitabadilika na itaendelea kubakia kama Ujerumani.
Merkel alisema kwamba ni wazi kabisa Ujerumani ni nchi madhubuti na dhamira yeo inapaswa kuwa tayari wameweza kumudu mambo mengi kwa hiyo wanaweza kumudu suala la wakimbizi na iwapo watakuwa na vizingiti njiani hawana budi kuvishinda na nchi itafanya kila iwezalo kwa kushirikiana na serikali za majimbo kufanikisha jambo hilo.
Ilikuwa ni tarehe 31 mwezi wa Augusti mwaka 2015 wakati Kansela Angela alipotowa kauli yake hiyo mashuhuri "wir schaffen das" tutalimudu hili wakati Ujerumani ilipowakaribisha mamia kwa maelfu ya wakimbizi na wahamiaji nchini waliokuwa wakikimbia vita na mizozo nchini mwao.
Akizungumza katika mahojiano na gazeti la Ujerumani la Sueddeutsche Zeitung yaliyochapishwa leo juu ya kauli mbiu yake hiyo ambayo imewagawa wananchi wa Ujerumani kimtizamo Merkel amesisitiza kwamba inaendelea kubakia kiini sahihi kwa jukumu la kukabiliana na mzozo huo.
Kansela Merkel ambaye kwa miezi kadhaa alikabiliwa na shutuma kwa kuonyesha moyo huo wa kujiamini kwa matumaini katika kuwashughulikia wakimbizi ameliambia gazeti hilo la Ujerumani kwamba Ujerumani na mataifa mengine ya Umoja wa Ulaya yalishindwa kuchukuwa hatua licha ya kuwepo kwa ushahidi ya mzozo huo kuzidi kuwa mkubwa.
Makosa yamefanyika
Merkerl amesema kuna masuala ya kisiasa ambayo mtu anaweza kuyaona kuwa yanakuja lakini kwa wakati fulani hayawaingii watu akilini na nchini Ujerumani wamelipuuza tatizo hilo kwa muda mrefu halikadhalika kuzuwiya hata na haja ya kutafutafuta usuluhishi wa umajumui wa Ulaya. Ameongeza kusema kwamba Ujerumani kwa miaka kadhaa imekuwa pia ikifanya makosa kwa kupinga mpango wa kugawana wakimbizi kwa uwiano na kulitupia jukumu hilo idara ya mipaka ya majini ya Umoja wa Ulaya.
Merkel amesema wakimbizi wengi walikuja mwaka 2004 na mwaka 2005 na wakaiwachilia Uhispania na wengine wa Idara ya Umoja wa Ulaya ya masuala ya mipaka ya nje kuwashughulikia. Amesema Ujerumani ilikuwa na furaha sana kwamba baada ya kupokea wakimbizi wengi wakati wa vita nchini Yugoslavia nchi nyengine sasa zilikuwa zinastahiki kulishughulikia suala hilo amesema jambo hilo hawezi kulikanusha.
Katika mahojiano hayo Merkel pia amekaririwa akisema "Ujerumani itabakia kuwa Ujerumani ikiwa na kila kitu ambacho inakipenda "
Ameongeza kusema mabadiliko yamekuwa yakitokea kwa miongo mingi lakini mabadiliko sio kitu kibaya yanahitajika katika maisha jambo lililo wazi ni kwamba Ujerumani haitoyaacha maadili yake.
Ugaidi hauletwi na wakimbizi
Kansela Merkel pia ameyatumia mahojiano hayo kuwashutumu wanasiasa wa Ujerumani kwa kuwataka wasitumie lugha kali na wasishiriki kupalilia kauli kwamba vitisho vinatoka nje.
Merkel ni "wazi sio sahihi kwamba ugaidi unaletwa na wakimbizi " na kwamba " tayari ulikuwepo hapa katika aina mbali mbali na kwamba wanaotaka kufanya mashambulizi wamekuwa wakisubiri kufanya hivyo."
Merkel na Halmashauri ya Umoja wa Ulaya wameshindwa kupiga hatua kubwa katika juhudi za kuyashirikisha mataiafa mengine ya Umoja wa Ulaya kugawana mzigo wa wakimbizi wanaowasili hivi sasa. DW

Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi Gabon

No comments:


Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi nchini Bongo
Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi nchini Bongo
Wanachama wa tume ya Uchaguzi mkuu nchini Gabon wametangaza kuwa rais Ali Bongo, amehifadhi kiti chake cha urais baada ya kumshinda mpinzani wake Jean Ping.
Ushindi huo ni baada ya kumalizika kwa shughuli za upigaji kura, hapo siku ya Jumamosi.
Lakini mwaandishi wa habari wa BBC mjini Libreville, amesema kuwa wajumbe wanaowakilisha upinzani katika tume ya uchaguzi, wameondoka ndani ya ukumbi wa kuhesabu na kusawazisha matokeo ya kura, na kukataa kutia saini hati zinazompa ushindi rais Bongo.
Walinda usalama wanapiga doria katika barabara za mji mkuu Libreville huku taharuki ikitanda kote nchini humo.
Familia ya Bongo imetawala Gabon kwa nusu karne huku Omar Bongo akitawala kwa miongo minne, na mwanawe rais wa sasa Ali, alichukua hatamu za uongozi mnamo mwaka wa 2009.BBC

MADEREVA BODABODA WAASWA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUJILETEA MAENDELEO

No comments:



unnamed
Mwenyekiti wa Muungano wa Vyama vya Waendesha Bodaboda  Dar es Salaam Bw. A. Leonard Mdede(wapilikutokakushoto) akizungumza na waandishi wahabari kuhusu waendesha Bodaboda kutojihusisha na mamandamano ya UKUTA Jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Michael Maiko,Mapinduzi Mpema na Said Kagambo.
Na Eleuteri Mangi, MAELEZO
VIONGOZI wa madereva waendesha bodaboda mkoa wa Dar es salaam wamewaasa wanachama wao kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo ya nchi kwa manufaa ya Watanzania wote.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti waendesha bodaboda kutoka Manispaa ya Kinondoni mkoani Dar es salaam Almano Mdede wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu utendaji wao wa kazi za kila siku.
Viongozi hao wamesema kuwa wanaimani na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika uongozi wake kwa dhamira yake ya kuwatumikia Watanzania na kuwataka madereva bodaboda wenzao kuendelea na majukumu yao ya kila siku ya kuwahudumia wananchi kwa kutoa huduma ya usafiri katika maeneo yao.
 “Ninawaomba wanachama wa chama cha maererva bodaboda mkoa wa Dar es salaam tutambue kuwa sisi ni wafanyabiashara kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tafadhali tumpe sekunde aweze kutekeleza aliyoahidi kwa Watanzania” alisema Mdede.
Aidha, Mdede alisema kuwa waendesha bodaboda hao ni wafanyabiashara kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo ni vema wafanye biashara kulingana na leseni zao.
Naye Mjumbe wa madereva wa bodaboda kutoka Kinondoni Oscar Waluye alisema kuwa waendesha bodaboda ambao ni wanachama katika umoja wao ni wale waliosajiliwa na kufanya biashara kwa kuzingatia leseni zao ambapo utambulisho wao unatokana na namba zao za pikipiki ambazo zimesajiliwa kwa “plate number” nyeupe na namba za usajili zimeandikwa kwa rangi nyeusi.
Aidha, madereva hao wamewaomba madereva bodaboda wenzao nchi nzima kupitia viongozi wao kuendelea kushirikiana na Serikali ili kujiletea maendeleo yao wenyewe na familia zao na taifa kwa ujumla. (P.T)

ALICHOKISEMA ALIYEKUWA KATIBU WA CHADEMA MKOANI MWANZA BAADA YA KUTIMKIA CCM

No comments:


1
Aliyekuwa Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema mkoani Mwanza, John Nzwalile (kulia), akirejesha kadi ya chama hicho kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo katika ofisi za CCM jana.
Na BMG
Nzwalile ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu Chadema Taifa, Mjumbe Baraza Kuu Chadema Taifa, Mwenyekiti wa Baraza la Mashauriano Chadema Mkoa wa Mwanza, amefikia uamuzi huo baada ya jana kujivua vyeo hivyo.
Amesema amefikia hatua hiyo kutokana na kwamba Chadema imepoteza mwelekeo kwani kimekuwa kikiibuka na oparesheni za kuichonganisha serikali na wananchi huku pia demokrasia ikikosekana ndani ya chama hicho.
“Kama ni udikiteta basi mimi niseme Chadema ndiko kuna udikiteta kwani zaidi ya mara tatu nimemsikia Lowasa (Edward Lowasa, aliyekuwa mgombea urais 2015) akisema yeye ndiye mgombea urais mwaka 2020, kwa kikao gani”. Amesema Nzwalile na kuongeza kwamba yale mambo yote mabaya yaliyokuwa yakifanyika ndani ya CCM yamenyooshwa hivyo hakuna haja ya yeye kuendelea kukaa Chadema.
Amesema atazunguka Wilaya zote ili kuhakikisha anawarejesha wengine ndani ya CCM huku akiwa na jukumu moja la kuubomoa Ukuta unaoelezwa kujengwa na Chadema kwani ni ukuta wa tope hivyo atatumia tu maji kuubomoa.
Nzwalile amekaribishwa ndani ya CCM na Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo, ambaye pia amewakaribisha makada wengine wa upinzani kuhamia CCM akisema kwamba chama hicho kinaendesha mambo yake kidemokrasia.

Mwenyekiti wa CCM mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo (kushoto) akipokea kadi ya Chadema ya aliyekuwa Katibu wa Chadema mkoani Mwanza, John Nzwalile (katikati).

Mwenyekiti wa CCM mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo (kushoto) akimkabidhi kadi ya CCM aliyekuwa Katibu wa Chadema mkoani Mwanza, John Nzwalile (kulia).
 

YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA PILI WA MWAKA WA NCHI 7 ZA AFRIKA MASHARIKI ZILIZO KATIKA MAPAMBANO YA KUTOKOMEZA TRAKOMA JIJINI ARUSHA

No comments:



Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya Kupambana na Trakoma (ITI) akizungumza na washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma kuhusu uendelezaji wa juhudi za kuwaelimisha wananchi na kutoa tiba katika maeneo  yanakabiliwa na ugonjwa Trakoma kwa nchi washiriki wa mkutano huo kutoka Kenya, Tanzania, Uganda, Ethiopia, Eritrea, Sudani na Sudani Kusini.

Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Upendo John Mwingira akiwasilisha kuhusu mkakati wa kukabiliana na Trakoma kwa kuyafikia maeneo yasiyofikika kirahisi ya jamii za wafugaji nchini Tanzania wakati Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo  unaofanyika  jijini Arusha. Wananchi kutoka Jamii za wafugaji kutoka nchi washiriki wa mkutano huo bado wanakabiliwa na changamoto ya ugonjwa wa Trakoma.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Frida Mokiti akichangia wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Mshiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma Kutoka nchini Kenya Dkt. Rebecca Oenga akitoa uzoefu wa nchi ya Kenya katika kukabiliana na Trakoma  kwenye maeneo ya mipakani  ya jamii za wafugaji.
Afisa Afya kutoka Kaunti ya NAROK nchini Kenya Daniel Sironka akitoa mchango wake kuhusu namna anavyowaelimisha wananchi wa eneo lake kujikinga na kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la Sightsavers, Michael Kelly (katikati) akisisitiza jambo kuhusu ushiriki wa Sightsavers katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakati wa mkutano wa pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Arusha.
 Washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Arusha.


Washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma kutoka Tanzania wakiwa katika majadiliano kabla ya kuwasilisha taarifa ya pamoja kuhusu maeneo ya utekelezaji katika mapambano dhidi ya Trakoma.
Picha/Aron Msigwa –MAELEZO.

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA DINI

No comments:



Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Mrisho Gambo(katikati)akizungumza na Askofu wa Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto)  alipomtembelea ofisini kwake na kufanya mazungumzo nae akiwa ameambata na Mbunge wa Tanzania kwenye Bunge la Afrika Mashariki(Eala)Mheshimiwa Angela Kizigha.

Askofu wa Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mh.Mrisho Gambo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mheshimiwa Mrisho Gambo akiagana na Askofu wa Kanisa la Anglikan Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kulia)  baada ya mazungumzo yao.
Nteghenjwa Hosseah – Arusha


Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo ameendelea  na  ziara yake ya kujitambulisha kwa viongozi wa dini  ukiwa ni utaratibu aliojiwekea wa kukutana na viongozi  baada ya kuteuliwa kushika  wadhifa huo hivi karibuni.


Mh.Gambo amekutana na  Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Mchungaji  Solomon Masangwa , Askofu wa  Kanisa la Evangelistic Assemblies of God(EAGT) mkoa wa Arusha,Leonard Mwizarubi  na Askofu  Stanley Hotay wa Kanisa la Anglikana , Dayosisi ya Mount  Kilimanjaro.


Katika mazungumzo na viongozi hao kwa nyakati tofauti mbali na kujitambulisha aliwahakikisha dhamira ya serikali kulinda na kuheshimu uhuru na haki ya kuabudu ambayo imekuwepo nchini kwa muda mrefu ikiwa ni njia ya kuwa na taifa la watu wenye hofu ya Mungu.


Alisema kutokana na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Joseph  Magufuli kutaka kuwainua wananchi wa chini kupitia mapato ya ndani  halmashauri zimetenga asilimia 10 kutoka kwenye mapato hayo kwa ajili ya  mikopo yenye riba nafuu kwa Wanawake na Vijana wajasiriamali  zitakazowawezesha kufanya  shughuli za uzalishaji mali.


Amewataka  wawajulishe waumini wa dini zote na serikali iko tayari  kupanga utaratibu wa maafisa maendeleo ya Jamii na Vijana kupita na kutoa  elimu kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na madhehebu ya dini hili iwe inufaishe watu wote katika mkoa huu bila kujali itikadi za kidini wala kisiasa.


Askofu Stanley Hotay aliupongeza uongozi wa mkoa kuimarisha hali ya utulivu na kuomba vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo Mkuu wa mkoa ndiye Mwenyekiti wake kukabiliana na changamoto za kiusalama na viashiria vya uvunjifu wa amani.



Aidha alishauri  kutokana na idadi ya watu wanaotumia usafiri wa anga kuongezeka kuna haja ya Serikali kufikiria uwezekano wa kupanua zaidi uwanja wa ndege wa Arusha uliopo Kisongo  ili uweze kukidhi mahitaji ya sasa badala ya kutegemea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) pekee.


Mh. Gambo amewahakikishia viongozi hao kuwa serikali itakua ikiwashirikisha mipango mbalimbali inayokusudia kuitekeleza ili  watoe mawazo yao katika kuiboresha na  kuifanya itekelezeke   kwa wepesi zaidi.

TAMASHA LA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA KASKAZINI KUFANYIKA SEPTEMBER 11, 2016

No comments:



Image result for TAMASHA LA TASWA ARUSHA  
Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha 
Bw. Mussa Juma  akiongea na waandishi wa habari


Na Woinde Shizza, Arusha
Chama cha waandishi wa habari za michezo na Burudanimkoa wa Arusha (TASWA ARUSHA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Arusha Media wameandaa  tamasha la 11 la  waandishi wa habari za michezo na burudani kanda ya Kaskazini ambalo litafanyika Septemba 11, 2016  katika uwanja wa Generat Tyre.
Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma alisema zaidi ya watu 2500 wanatarajiwa kushiriki Tamasha hilo, ambapo kutakuwa na michezo ya Soka, Kuvuta kamba, Mbio za magunia ,Kukimbiza kuku na muziki kuanzia saa nne asubuhi hadi jioni.
Juma alizitaja timu ambazo zitashiriki ni TASWA FC kutoka jijini Dar es Salaam, timu ya Radio  ORS kutoka mkoa wa Manyara, timu ya Sunrise Radio, Timu ya chuo cha uandishi habari Arusha, timu ya MJ Radio na timu ya Triple a Radio.

Katika tamasha hilo, pia kutakuwa na timu za vyuo vya uandishi habari vya mkoa wa Arusha, chuo cha habari Maalum, Tasisi ya habari na mawasiliano iliyopo maji ya chai, TASWA Arusha.

“tamasha litatanguliwa na semina ya siku moja ya wanahabari mkoani Arusha juu ya masuala ya michezo, Utalii wa ndani na umuhimu wa Uwekezaji katika taifa”alisema.

Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea  Ngobole alifafanua kuwa pia kuna timu ambazo zimealikwa ambazo ni Kitambi Noma, Timu ya TANAPA,timu ya TBL Arusha, timu ya PEPSI na Coca Cola na  Wenyeji  timu ya Wazee Klabu.

Ngobole alisema Septemba 3, TASWA na Arusha Media watatangaza zawadi kwa washindi, wadhamini wote na Mgeni rasmi.

CHRISTIAN BELLA KUWASHA MOTO SHINDANO LA MISS KINONDONI 2016, KESHO KUTWA UKUMBI WA DENFRANCES SINZA JIJINI DAR ES SALAAM

No comments:


Washiriki wa shindano la  Lete Raha Miss Kinondoni 2016 wakishuka kwenye gari Dar es Salaam jana walipofanya ziara ya kutembelea Makao Makuu ya Mdhamini wao Kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd Mikocheni.
Wanyange hao 20 wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya 
gari la kampuni hiyo.
Meneja wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd, Mr Rutha akizungumza na wanyange hao walipotembelea makao makuu ya Kampuni hiyo Mikochezni Dar es Salaam jana.
Warembo hao wakiwa mbele ya ghala zinamo hifadhiwa bia za Windhoek wakati wa ziara hiyo.
Warembo hao wakisubiri mkutano na wanahabari baada ya ziara hiyo.

Mshauri wa Miss Kinondoni, Boy George (katikati), akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya shindano hilo. Kutoka kulia ni Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Mabibo,Constantine Mwafulilwa, Andrea Missana, Mratibu wa Shindani la Miss Kinondoni Rhamat George na Mwalimu wa warembo hao, Neema Chaky.
Maofisa wa Kampuni ya Mabibo wakiwa katika pozi. Kutoka kushoto ni, Mr Jerome, Ismail Mzava na Mr Rutha.
Mwalimu wa Wanyange hao, Neema Chaky (kushoto), akizungumza katika mkutano huo.
Wanyange hao katika tabasamu.
Mratibu wa shindano hilo, Rhamat George (katikati), akizungumza katika mkutano huo.
Viongozim meza kuu na wanyange hao wakionesha bia ya windhoek.

Na Dotto Mwaibale

Mwanamuziki nguri wa muziki wa dansi hapa nchini Cristian Bella anatarajiwa kuwasha moto katika shindano la kumsaka Malkia wa Ulimbwende.
Kanda ya Kinondoni linatarajiwa kufanyika kesho kutwa Ijumaaya katika Ukumbi wa Denfrances Sinza jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kuwa kutanisha warembo hao  na wadhamini washindano hilo ambao ni Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd ambao ni wasambaji wa kinywaji cha Windhoek Dar es Salaam jana, Ofisa Mauzo wa kampuni hiyo, Andrea Misama alisema maandalizi ya shindano hilo yanaendalea vizuri ambapo aliwashukuru warembo wote waliojitokeza kwenye shindano hilo kwa mwaka huu na kuwa mwanamuziki huyo akishirikiana na kundi la sanaa la kampuni hiyo watapamba jukwaa kwa kutoa burudani la kukata na shoka.

"Mwaka huu washiriki waliojitokeza ni wengi ukulinganisha na mwaka jana, hivyo tunatoa pongezi kwa wazazi waliowaruhusu watoto wao kushiriki, malengo yetu ni kukuza vipaji na kutoa ajira kwa wasichana ili waweze kutimiza ndoto zao”,  alisema.

Kwa pande wao warembo watakaoshiriki shindano hilo wameahidi kuonyesha vipaji walivyonavyo na kuwaomba wadau na mashabiki waurembo kujitokeza kwa wingi siku ya shindano ili wawezekusapoti Miss Kinondoni.

Shindano hilo linashirikisha warembo 20 kutoka vitongoji mbalimbali vya Kanda ya Kinondoni ambapo kiingilio kitakuwa sh 10,000 na 20,000 kwa VIP huku shindano hilo likipambwa kwa burudani kutoka kwa mkali wa masauti Christian Bella.

MWENYEKITI WA BODI YA UTALII (TTB) AWAAGA WATALII NA WAANDISHI WA HABARI WANAOKWENDA RUJEWA KUSHUHUDIA KUPATWA KWA JUA

No comments:


1
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas Mihayo akiagana na Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena Kiongozi wa Msafara wa Watalii wa Ndani na waandishi wa habari wanaotoka Dar es salaam kwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua ambapo wageni mbalimbali pamoja na wanahabari kutoka vyombo vya habari vya ndani na vya kimataifa wako mkoani humo kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo nadra kutokea duniani.
2
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas Mihayo na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii TTB Bi. Devotha Mdachi wakiagana na Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena pamoja na Antonio Nugas Mtembezi kutoka Clouds Media Viongozi wa Msafara wa Watalii wa Ndani na waandishi wa habari wanaokwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
3
Baadhi ya wapiga picha wa vyombo vya habari hapa nchini wakiendelea na kazi yao wakati msafara huo ukiondoka jijini Dar es salaam.
4
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas Mihayo na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Bi. Devotha Mdachi wakielekea kwenye gari kwa ajili ya kuwaaga baadhi ya watalii wa Ndani na waandishi wa habari wanaokwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua wakitokea jijini Dar es salaam..
6

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas Mihayo akizungumza na waandishi wa habari na kuwapa maneno kadhaa wakati akiwaaga baadhi ya watalii wa Ndani na waandishi wa habari wanaokwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua wakitokea jijini Dar es salaam
7 8
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas Mihayo akizungumza na waandishi wa habari, kulia ni Bi. Devotha Mdachi Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii TTB na kutoka kushoto ni Mtangazaji wa Clouds Baby Kabaya na Mkurugenzi wa Masoko TTB Bw. Philip Chitaunga,
10
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas Mihayo akiasalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Utalii TTB.
12
Kulia ni Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena na kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TTB Bw. Geofrey Tengeneza na Mkurugenzi wa Masoko TTB Bw. Philip Chitaunga.
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger