Wednesday, August 31, 2016
RC ARUSHA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA DINI
Mkuu wa
mkoa wa Arusha,Mheshimiwa Mrisho Gambo(katikati)akizungumza na Askofu wa
Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto) alipomtembelea ofisini kwake
Askofu wa Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mh.Mrisho Gambo.
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mheshimiwa Mrisho Gambo akiagana na Askofu wa Kanisa la Anglikan Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kulia) baada ya mazungumzo yao.
Nteghenjwa Hosseah – Arusha
Mkuu
wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo ameendelea na ziara yake ya
kujitambulisha kwa viongozi wa dini ukiwa ni utaratibu aliojiwekea wa
kukutana na viongozi baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi
karibuni.
Mh.Gambo
amekutana na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri
Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Mchungaji Solomon
Masangwa , Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God(EAGT)
mkoa wa Arusha,Leonard Mwizarubi na Askofu Stanley Hotay wa Kanisa la
Anglikana , Dayosisi ya Mount
Kilimanjaro.
Kilimanjaro.
Katika
mazungumzo na viongozi hao kwa nyakati tofauti mbali na kujitambulisha
aliwahakikisha dhamira ya serikali kulinda na kuheshimu uhuru na haki ya
kuabudu ambayo imekuwepo nchini kwa muda mrefu ikiwa ni njia ya kuwa na
taifa la watu wenye hofu ya Mungu.
Alisema kutokana na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Joseph Magufuli
kutaka kuwainua wananchi wa chini kupitia mapato ya ndani halmashauri
zimetenga asilimia 10 kutoka kwenye mapato hayo kwa ajili ya mikopo
yenye riba nafuu kwa Wanawake na Vijana wajasiriamali zitakazowawezesha
kufanya shughuli za uzalishaji mali.
Amewataka wawajulishe waumini wa dini zote na serikali iko tayarikupanga utaratibu wa maafisa maendeleo ya Jamii na Vijana kupita na kutoa elimu
kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na madhehebu ya dini hili iwe
inufaishe watu wote katika mkoa huu bila kujali itikadi za kidini wala
kisiasa.
Askofu
Stanley Hotay aliupongeza uongozi wa mkoa kuimarisha hali ya utulivu na
kuomba vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo Mkuu wa mkoa ndiye
Mwenyekiti wake kukabiliana na changamoto za kiusalama na viashiria vya
uvunjifu wa amani.
Aidha alishauri kutokana
na idadi ya watu wanaotumia usafiri wa anga kuongezeka kuna haja ya
Serikali kufikiria uwezekano wa kupanua zaidi uwanja wa ndege wa Arusha
uliopo Kisongo ili uweze kukidhi mahitaji ya sasa badala ya kutegemea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) pekee.
Mh.
Gambo amewahakikishia viongozi hao kuwa serikali itakua ikiwashirikisha
mipango mbalimbali inayokusudia kuitekeleza ili watoe mawazo yao
katika kuiboresha na kuifanya itekelezeke kwa wepesi zaidi.(P.T)
Merkel : Makosa yalifanyika katika suala la wakimbizi
Kansela
Angela Merkel wa Ujerumani amekiri kumefanyika makosa Ujerumani na Umoja
wa Ulaya katika suala la mzozo wa wakimbizi lakini amesisitiza kwamba
Ujerumani haitabadilika na itaendelea kubakia kama Ujerumani.
Merkel
alisema kwamba ni wazi kabisa Ujerumani ni nchi madhubuti na dhamira yeo
inapaswa kuwa tayari wameweza kumudu mambo mengi kwa hiyo wanaweza
kumudu suala la wakimbizi na iwapo watakuwa na vizingiti njiani hawana
budi kuvishinda na nchi itafanya kila iwezalo kwa kushirikiana na
serikali za majimbo kufanikisha jambo hilo.
Ilikuwa
ni tarehe 31 mwezi wa Augusti mwaka 2015 wakati Kansela Angela alipotowa
kauli yake hiyo mashuhuri "wir schaffen das" tutalimudu hili wakati
Ujerumani ilipowakaribisha mamia kwa maelfu ya wakimbizi na wahamiaji
nchini waliokuwa wakikimbia vita na mizozo nchini mwao.
Akizungumza
katika mahojiano na gazeti la Ujerumani la Sueddeutsche Zeitung
yaliyochapishwa leo juu ya kauli mbiu yake hiyo ambayo imewagawa
wananchi wa Ujerumani kimtizamo Merkel amesisitiza kwamba inaendelea
kubakia kiini sahihi kwa jukumu la kukabiliana na mzozo huo.
Kansela
Merkel ambaye kwa miezi kadhaa alikabiliwa na shutuma kwa kuonyesha moyo
huo wa kujiamini kwa matumaini katika kuwashughulikia wakimbizi
ameliambia gazeti hilo la Ujerumani kwamba Ujerumani na mataifa mengine
ya Umoja wa Ulaya yalishindwa kuchukuwa hatua licha ya kuwepo kwa
ushahidi ya mzozo huo kuzidi kuwa mkubwa.
Makosa yamefanyika
Merkerl
amesema kuna masuala ya kisiasa ambayo mtu anaweza kuyaona kuwa yanakuja
lakini kwa wakati fulani hayawaingii watu akilini na nchini Ujerumani
wamelipuuza tatizo hilo kwa muda mrefu halikadhalika kuzuwiya hata na
haja ya kutafutafuta usuluhishi wa umajumui wa Ulaya. Ameongeza kusema
kwamba Ujerumani kwa miaka kadhaa imekuwa pia ikifanya makosa kwa
kupinga mpango wa kugawana wakimbizi kwa uwiano na kulitupia jukumu hilo
idara ya mipaka ya majini ya Umoja wa Ulaya.
Merkel
amesema wakimbizi wengi walikuja mwaka 2004 na mwaka 2005 na
wakaiwachilia Uhispania na wengine wa Idara ya Umoja wa Ulaya ya masuala
ya mipaka ya nje kuwashughulikia. Amesema Ujerumani ilikuwa na furaha
sana kwamba baada ya kupokea wakimbizi wengi wakati wa vita nchini
Yugoslavia nchi nyengine sasa zilikuwa zinastahiki kulishughulikia suala
hilo amesema jambo hilo hawezi kulikanusha.
Katika mahojiano hayo Merkel pia amekaririwa akisema "Ujerumani itabakia kuwa Ujerumani ikiwa na kila kitu ambacho inakipenda "
Ameongeza
kusema mabadiliko yamekuwa yakitokea kwa miongo mingi lakini mabadiliko
sio kitu kibaya yanahitajika katika maisha jambo lililo wazi ni kwamba
Ujerumani haitoyaacha maadili yake.
Ugaidi hauletwi na wakimbizi
Kansela
Merkel pia ameyatumia mahojiano hayo kuwashutumu wanasiasa wa Ujerumani
kwa kuwataka wasitumie lugha kali na wasishiriki kupalilia kauli kwamba
vitisho vinatoka nje.
Merkel ni
"wazi sio sahihi kwamba ugaidi unaletwa na wakimbizi " na kwamba "
tayari ulikuwepo hapa katika aina mbali mbali na kwamba wanaotaka
kufanya mashambulizi wamekuwa wakisubiri kufanya hivyo."
Merkel na
Halmashauri ya Umoja wa Ulaya wameshindwa kupiga hatua kubwa katika
juhudi za kuyashirikisha mataiafa mengine ya Umoja wa Ulaya kugawana
mzigo wa wakimbizi wanaowasili hivi sasa. DW
Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi Gabon
Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi nchini Bongo
Wanachama
wa tume ya Uchaguzi mkuu nchini Gabon wametangaza kuwa rais Ali Bongo,
amehifadhi kiti chake cha urais baada ya kumshinda mpinzani wake Jean
Ping.
Ushindi huo ni baada ya kumalizika kwa shughuli za upigaji kura, hapo siku ya Jumamosi.
Lakini
mwaandishi wa habari wa BBC mjini Libreville, amesema kuwa wajumbe
wanaowakilisha upinzani katika tume ya uchaguzi, wameondoka ndani ya
ukumbi wa kuhesabu na kusawazisha matokeo ya kura, na kukataa kutia
saini hati zinazompa ushindi rais Bongo.
Walinda usalama wanapiga doria katika barabara za mji mkuu Libreville huku taharuki ikitanda kote nchini humo.
Familia
ya Bongo imetawala Gabon kwa nusu karne huku Omar Bongo akitawala kwa
miongo minne, na mwanawe rais wa sasa Ali, alichukua hatamu za uongozi
mnamo mwaka wa 2009.BBC
MADEREVA BODABODA WAASWA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUJILETEA MAENDELEO
Mwenyekiti
wa Muungano wa Vyama vya Waendesha Bodaboda Dar es Salaam Bw. A.
Leonard Mdede(wapilikutokakushoto) akizungumza na waandishi wahabari
kuhusu waendesha Bodaboda kutojihusisha na mamandamano ya UKUTA Jijini
Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Michael Maiko,Mapinduzi Mpema na Said
Kagambo.
Na Eleuteri Mangi, MAELEZO
VIONGOZI
wa madereva waendesha bodaboda mkoa wa Dar es salaam wamewaasa wanachama
wao kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo ya nchi
kwa manufaa ya Watanzania wote.
Hayo
yamesemwa na Mwenyekiti waendesha bodaboda kutoka Manispaa ya Kinondoni
mkoani Dar es salaam Almano Mdede wakati akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es salaam kuhusu utendaji wao wa kazi za kila siku.
Viongozi
hao wamesema kuwa wanaimani na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika
uongozi wake kwa dhamira yake ya kuwatumikia Watanzania na kuwataka
madereva bodaboda wenzao kuendelea na majukumu yao ya kila siku ya
kuwahudumia wananchi kwa kutoa huduma ya usafiri katika maeneo yao.
“Ninawaomba
wanachama wa chama cha maererva bodaboda mkoa wa Dar es salaam tutambue
kuwa sisi ni wafanyabiashara kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, tafadhali tumpe sekunde aweze kutekeleza
aliyoahidi kwa Watanzania” alisema Mdede.
Aidha,
Mdede alisema kuwa waendesha bodaboda hao ni wafanyabiashara kwa mujibu
wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo ni vema wafanye
biashara kulingana na leseni zao.
Naye
Mjumbe wa madereva wa bodaboda kutoka Kinondoni Oscar Waluye alisema
kuwa waendesha bodaboda ambao ni wanachama katika umoja wao ni wale
waliosajiliwa na kufanya biashara kwa kuzingatia leseni zao ambapo
utambulisho wao unatokana na namba zao za pikipiki ambazo zimesajiliwa
kwa “plate number” nyeupe na namba za usajili zimeandikwa kwa rangi
nyeusi.
Aidha,
madereva hao wamewaomba madereva bodaboda wenzao nchi nzima kupitia
viongozi wao kuendelea kushirikiana na Serikali ili kujiletea maendeleo
yao wenyewe na familia zao na taifa kwa ujumla. (P.T)
ALICHOKISEMA ALIYEKUWA KATIBU WA CHADEMA MKOANI MWANZA BAADA YA KUTIMKIA CCM
Aliyekuwa
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema mkoani Mwanza, John
Nzwalile (kulia), akirejesha kadi ya chama hicho kwa Mwenyekiti wa
Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo katika ofisi za
CCM jana.
Na BMG
Nzwalile
ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu Chadema Taifa, Mjumbe Baraza
Kuu Chadema Taifa, Mwenyekiti wa Baraza la Mashauriano Chadema Mkoa wa
Mwanza, amefikia uamuzi huo baada ya jana kujivua vyeo hivyo.
Amesema
amefikia hatua hiyo kutokana na kwamba Chadema imepoteza mwelekeo kwani
kimekuwa kikiibuka na oparesheni za kuichonganisha serikali na wananchi
huku pia demokrasia ikikosekana ndani ya chama hicho.
“Kama ni
udikiteta basi mimi niseme Chadema ndiko kuna udikiteta kwani zaidi ya
mara tatu nimemsikia Lowasa (Edward Lowasa, aliyekuwa mgombea urais
2015) akisema yeye ndiye mgombea urais mwaka 2020, kwa kikao gani”.
Amesema Nzwalile na kuongeza kwamba yale mambo yote mabaya yaliyokuwa
yakifanyika ndani ya CCM yamenyooshwa hivyo hakuna haja ya yeye
kuendelea kukaa Chadema.
Amesema
atazunguka Wilaya zote ili kuhakikisha anawarejesha wengine ndani ya CCM
huku akiwa na jukumu moja la kuubomoa Ukuta unaoelezwa kujengwa na
Chadema kwani ni ukuta wa tope hivyo atatumia tu maji kuubomoa.
Nzwalile
amekaribishwa ndani ya CCM na Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani Mwanza,
Dkt.Antony Diallo, ambaye pia amewakaribisha makada wengine wa upinzani
kuhamia CCM akisema kwamba chama hicho kinaendesha mambo yake
kidemokrasia.
Mwenyekiti
wa CCM mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo (kushoto) akipokea kadi ya
Chadema ya aliyekuwa Katibu wa Chadema mkoani Mwanza, John Nzwalile
(katikati).
Mwenyekiti
wa CCM mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo (kushoto) akimkabidhi kadi ya
CCM aliyekuwa Katibu wa Chadema mkoani Mwanza, John Nzwalile (kulia).
YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA PILI WA MWAKA WA NCHI 7 ZA AFRIKA MASHARIKI ZILIZO KATIKA MAPAMBANO YA KUTOKOMEZA TRAKOMA JIJINI ARUSHA
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Kimataifa ya Kupambana na Trakoma (ITI) akizungumza na washiriki
wa mkutano wa
pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya
ugonjwa wa Trakoma kuhusu uendelezaji wa juhudi za
kuwaelimisha wananchi na kutoa tiba katika maeneo yanakabiliwa na ugonjwa Trakoma kwa nchi
washiriki wa mkutano huo kutoka Kenya, Tanzania, Uganda, Ethiopia, Eritrea,
Sudani na Sudani Kusini.
Mratibu wa Taifa wa
Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Upendo John Mwingira akiwasilisha
kuhusu mkakati wa kukabiliana na Trakoma kwa kuyafikia maeneo yasiyofikika
kirahisi ya jamii za wafugaji nchini Tanzania wakati Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7
za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo unaofanyika
jijini Arusha. Wananchi kutoka Jamii za wafugaji kutoka nchi washiriki
wa mkutano huo bado wanakabiliwa na changamoto ya
ugonjwa wa Trakoma.
Mganga
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Frida Mokiti akichangia wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za
Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini
Arusha.
Mshiriki wa mkutano wa pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa
Trakoma Kutoka nchini Kenya Dkt. Rebecca Oenga akitoa uzoefu wa nchi ya Kenya
katika kukabiliana na Trakoma kwenye
maeneo ya mipakani ya jamii za wafugaji.
Afisa Afya kutoka Kaunti ya NAROK
nchini Kenya Daniel Sironka akitoa mchango wake kuhusu namna anavyowaelimisha
wananchi wa eneo lake kujikinga na kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa
Trakoma wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo
katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la Sightsavers,
Michael Kelly (katikati) akisisitiza jambo kuhusu ushiriki wa Sightsavers
katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakati wa mkutano
wa
pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki
zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Washiriki wa mkutano wa pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa
Trakoma wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Arusha.
Washiriki wa mkutano wa pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa
Trakoma wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Arusha.
Washiriki wa mkutano wa pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa
Trakoma kutoka Tanzania wakiwa katika majadiliano kabla ya kuwasilisha taarifa
ya pamoja kuhusu maeneo ya utekelezaji katika mapambano dhidi ya Trakoma.
Picha/Aron Msigwa –MAELEZO.
MKUU WA MKOA WA ARUSHA AFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA DINI
Askofu wa Kanisa la Anglikan,Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kushoto) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mh.Mrisho Gambo. |
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mheshimiwa Mrisho Gambo akiagana na Askofu wa Kanisa la Anglikan Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay(kulia) baada ya mazungumzo yao. |
Nteghenjwa Hosseah – Arusha
Mkuu wa mkoa wa
Arusha,Mrisho Gambo ameendelea na ziara yake ya kujitambulisha kwa
viongozi wa dini ukiwa ni utaratibu aliojiwekea wa kukutana na viongozi
baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni.
Mh.Gambo amekutana na
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini
Kati,Mchungaji Solomon Masangwa , Askofu wa Kanisa la
Evangelistic Assemblies of God(EAGT) mkoa wa Arusha,Leonard Mwizarubi na
Askofu Stanley Hotay wa Kanisa la Anglikana , Dayosisi ya Mount
Kilimanjaro.
Katika mazungumzo na
viongozi hao kwa nyakati tofauti mbali na kujitambulisha aliwahakikisha dhamira
ya serikali kulinda na kuheshimu uhuru na haki ya kuabudu ambayo imekuwepo
nchini kwa muda mrefu ikiwa ni njia ya kuwa na taifa la watu wenye hofu ya
Mungu.
Alisema kutokana na
serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Joseph Magufuli kutaka kuwainua wananchi wa chini
kupitia mapato ya ndani halmashauri zimetenga asilimia 10 kutoka kwenye
mapato hayo kwa ajili ya mikopo yenye riba nafuu kwa Wanawake na Vijana
wajasiriamali zitakazowawezesha kufanya shughuli za uzalishaji
mali.
Amewataka wawajulishe waumini wa dini zote na serikali
iko tayari kupanga utaratibu wa maafisa
maendeleo ya Jamii na Vijana kupita na kutoa
elimu kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na madhehebu ya dini hili iwe
inufaishe watu wote katika mkoa huu bila kujali itikadi za kidini wala kisiasa.
Askofu Stanley Hotay
aliupongeza uongozi wa mkoa kuimarisha hali ya utulivu na kuomba vyombo vya
ulinzi na usalama ambavyo Mkuu wa mkoa ndiye Mwenyekiti wake kukabiliana na
changamoto za kiusalama na viashiria vya uvunjifu wa amani.
Aidha alishauri kutokana na idadi ya watu wanaotumia usafiri
wa anga kuongezeka kuna haja ya Serikali kufikiria uwezekano wa kupanua zaidi
uwanja wa ndege wa Arusha uliopo Kisongo ili uweze kukidhi mahitaji ya sasa badala ya
kutegemea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) pekee.
Mh. Gambo amewahakikishia
viongozi hao kuwa serikali itakua ikiwashirikisha mipango mbalimbali
inayokusudia kuitekeleza ili watoe mawazo yao katika kuiboresha na kuifanya
itekelezeke kwa wepesi zaidi.
TAMASHA LA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA KASKAZINI KUFANYIKA SEPTEMBER 11, 2016
Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha
Bw. Mussa Juma akiongea na waandishi wa habari
Bw. Mussa Juma akiongea na waandishi wa habari
Na Woinde Shizza, Arusha
Chama
cha waandishi wa habari za michezo na Burudanimkoa wa Arusha (TASWA
ARUSHA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Arusha Media wameandaa tamasha
la 11 la waandishi wa habari za michezo na burudani kanda ya Kaskazini
ambalo litafanyika Septemba 11, 2016 katika uwanja wa Generat Tyre.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma
alisema zaidi ya watu 2500 wanatarajiwa kushiriki Tamasha hilo, ambapo
kutakuwa na michezo ya Soka, Kuvuta kamba, Mbio za magunia ,Kukimbiza
kuku na muziki kuanzia saa nne asubuhi hadi jioni.
Juma
alizitaja timu ambazo zitashiriki ni TASWA FC kutoka jijini Dar es
Salaam, timu ya Radio ORS kutoka mkoa wa Manyara, timu ya Sunrise
Radio, Timu ya chuo cha uandishi habari Arusha, timu ya MJ Radio na timu
ya Triple a Radio.
Katika
tamasha hilo, pia kutakuwa na timu za vyuo vya uandishi habari vya mkoa
wa Arusha, chuo cha habari Maalum, Tasisi ya habari na mawasiliano
iliyopo maji ya chai, TASWA Arusha.
“tamasha
litatanguliwa na semina ya siku moja ya wanahabari mkoani Arusha juu ya
masuala ya michezo, Utalii wa ndani na umuhimu wa Uwekezaji katika
taifa”alisema.
Mratibu
wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole alifafanua kuwa pia kuna timu ambazo
zimealikwa ambazo ni Kitambi Noma, Timu ya TANAPA,timu ya TBL Arusha,
timu ya PEPSI na Coca Cola na Wenyeji timu ya Wazee Klabu.
Ngobole alisema Septemba 3, TASWA na Arusha Media watatangaza zawadi kwa washindi, wadhamini wote na Mgeni rasmi.
CHRISTIAN BELLA KUWASHA MOTO SHINDANO LA MISS KINONDONI 2016, KESHO KUTWA UKUMBI WA DENFRANCES SINZA JIJINI DAR ES SALAAM
Washiriki
wa shindano la Lete Raha Miss Kinondoni 2016 wakishuka kwenye gari Dar
es Salaam jana walipofanya ziara ya kutembelea Makao Makuu ya Mdhamini
wao Kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd Mikocheni.
Wanyange hao 20 wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya
gari la kampuni hiyo.
Meneja
wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd, Mr Rutha akizungumza
na wanyange hao walipotembelea makao makuu ya Kampuni hiyo Mikochezni
Dar es Salaam jana.
Warembo hao wakiwa mbele ya ghala zinamo hifadhiwa bia za Windhoek wakati wa ziara hiyo.
Warembo hao wakisubiri mkutano na wanahabari baada ya ziara hiyo.
Mshauri
wa Miss Kinondoni, Boy George (katikati), akizungumza kwenye mkutano na
waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya shindano hilo.
Kutoka kulia ni Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Mabibo,Constantine Mwafulilwa,
Andrea Missana, Mratibu wa Shindani la Miss Kinondoni Rhamat George na
Mwalimu wa warembo hao, Neema Chaky.
Maofisa wa Kampuni ya Mabibo wakiwa katika pozi. Kutoka kushoto ni, Mr Jerome, Ismail Mzava na Mr Rutha.
Mwalimu wa Wanyange hao, Neema Chaky (kushoto), akizungumza katika mkutano huo.
Wanyange hao katika tabasamu.
Mratibu wa shindano hilo, Rhamat George (katikati), akizungumza katika mkutano huo.
Viongozim meza kuu na wanyange hao wakionesha bia ya windhoek.
Na Dotto Mwaibale
Mwanamuziki nguri wa muziki wa dansi hapa nchini Cristian Bella anatarajiwa kuwasha moto katika shindano la kumsaka Malkia wa Ulimbwende.
Kanda ya Kinondoni linatarajiwa kufanyika kesho kutwa Ijumaaya katika Ukumbi wa Denfrances Sinza jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kuwa kutanisha warembo hao na wadhamini washindano hilo ambao ni Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd ambao ni wasambaji wa kinywaji cha Windhoek Dar es Salaam jana, Ofisa Mauzo wa kampuni hiyo, Andrea Misama alisema maandalizi ya shindano hilo yanaendalea vizuri ambapo aliwashukuru warembo wote waliojitokeza kwenye shindano hilo kwa mwaka huu na kuwa mwanamuziki huyo akishirikiana na kundi la sanaa la kampuni hiyo watapamba jukwaa kwa kutoa burudani la kukata na shoka.
"Mwaka huu washiriki waliojitokeza ni wengi ukulinganisha na mwaka jana, hivyo tunatoa pongezi kwa wazazi waliowaruhusu watoto wao kushiriki, malengo yetu ni kukuza vipaji na kutoa ajira kwa wasichana ili waweze kutimiza ndoto zao”, alisema.
Kwa pande wao warembo watakaoshiriki shindano hilo wameahidi kuonyesha vipaji walivyonavyo na kuwaomba wadau na mashabiki waurembo kujitokeza kwa wingi siku ya shindano ili wawezekusapoti Miss Kinondoni.
Shindano hilo linashirikisha warembo 20 kutoka vitongoji mbalimbali vya Kanda ya Kinondoni ambapo kiingilio kitakuwa sh 10,000 na 20,000 kwa VIP huku shindano hilo likipambwa kwa burudani kutoka kwa mkali wa masauti Christian Bella.
Na Dotto Mwaibale
Mwanamuziki nguri wa muziki wa dansi hapa nchini Cristian Bella anatarajiwa kuwasha moto katika shindano la kumsaka Malkia wa Ulimbwende.
Kanda ya Kinondoni linatarajiwa kufanyika kesho kutwa Ijumaaya katika Ukumbi wa Denfrances Sinza jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kuwa kutanisha warembo hao na wadhamini washindano hilo ambao ni Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd ambao ni wasambaji wa kinywaji cha Windhoek Dar es Salaam jana, Ofisa Mauzo wa kampuni hiyo, Andrea Misama alisema maandalizi ya shindano hilo yanaendalea vizuri ambapo aliwashukuru warembo wote waliojitokeza kwenye shindano hilo kwa mwaka huu na kuwa mwanamuziki huyo akishirikiana na kundi la sanaa la kampuni hiyo watapamba jukwaa kwa kutoa burudani la kukata na shoka.
"Mwaka huu washiriki waliojitokeza ni wengi ukulinganisha na mwaka jana, hivyo tunatoa pongezi kwa wazazi waliowaruhusu watoto wao kushiriki, malengo yetu ni kukuza vipaji na kutoa ajira kwa wasichana ili waweze kutimiza ndoto zao”, alisema.
Kwa pande wao warembo watakaoshiriki shindano hilo wameahidi kuonyesha vipaji walivyonavyo na kuwaomba wadau na mashabiki waurembo kujitokeza kwa wingi siku ya shindano ili wawezekusapoti Miss Kinondoni.
Shindano hilo linashirikisha warembo 20 kutoka vitongoji mbalimbali vya Kanda ya Kinondoni ambapo kiingilio kitakuwa sh 10,000 na 20,000 kwa VIP huku shindano hilo likipambwa kwa burudani kutoka kwa mkali wa masauti Christian Bella.
MWENYEKITI WA BODI YA UTALII (TTB) AWAAGA WATALII NA WAANDISHI WA HABARI WANAOKWENDA RUJEWA KUSHUHUDIA KUPATWA KWA JUA
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas
Mihayo akiagana na Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena Kiongozi wa
Msafara wa Watalii wa Ndani na waandishi wa habari wanaotoka Dar es
salaam kwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya
kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua ambapo wageni mbalimbali pamoja na
wanahabari kutoka vyombo vya habari vya ndani na vya kimataifa wako
mkoani humo kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo nadra kutokea duniani.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas
Mihayo na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii TTB Bi. Devotha Mdachi wakiagana
na Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena pamoja na Antonio Nugas
Mtembezi kutoka Clouds Media Viongozi wa Msafara wa Watalii wa Ndani na
waandishi wa habari wanaokwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya
kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
Baadhi
ya wapiga picha wa vyombo vya habari hapa nchini wakiendelea na kazi
yao wakati msafara huo ukiondoka jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas
Mihayo na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Bi. Devotha Mdachi wakielekea
kwenye gari kwa ajili ya kuwaaga baadhi ya watalii wa Ndani na waandishi
wa habari wanaokwenda Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili
ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua wakitokea jijini Dar es salaam..
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas
Mihayo akizungumza na waandishi wa habari na kuwapa maneno kadhaa wakati
akiwaaga baadhi ya watalii wa Ndani na waandishi wa habari wanaokwenda
Rujewa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya kushuhudia tukio la
kupatwa kwa jua wakitokea jijini Dar es salaam
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas
Mihayo akizungumza na waandishi wa habari, kulia ni Bi. Devotha Mdachi
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii TTB na kutoka kushoto ni Mtangazaji wa
Clouds Baby Kabaya na Mkurugenzi wa Masoko TTB Bw. Philip Chitaunga,
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania TTB Mh. Jaji Thomas
Mihayo akiasalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Utalii TTB.
Kulia
ni Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena na kutoka kushoto ni Mkuu wa
Kitengo cha Mawasiliano TTB Bw. Geofrey Tengeneza na Mkurugenzi wa
Masoko TTB Bw. Philip Chitaunga.
Subscribe to:
Posts (Atom)