TRA

TRA

Thursday, September 1, 2016

Ali Bongo alaani maandamano dhidi ya demokrasia

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


media
Rais Ali Bongo Ondimba katika mkutano na waandishi wa habari Septemba 1, 2016.
Rais wa Gabon Ali Bongo amesema Alhamisi hii kuwa "demokrasia enaeleweka vibaya kwa kuvamia na kushambulia jengo la Bunge. " Ujumbe wa Bw Bongo ulikua ukielekezwa kwa upinzani unaopinga kuchaguliwa kwake tena.
"Uchaguzi umetoa uamuzi wake. Ni nani aliyepoteza? Kundi dogo ambalo mpango wake ilikuwa kuchukua madaraka ili kunufaika kupitia nchi ya Gabon na wala sio kuitumika nchi ya Gabon,"amesema Ali Bongo wakati wa hotuba yake kwa vyombo vya habari.
Pia Waziri wa Mambo ya Ndani ametangaza kwamba maelfu raia wamekamatwa tangu Jumatano usiku.
"Katika mji wa Libreville pekee, watu kati ya 600 na 800 wamekamatwa, na 200 hadi 300 katika maeneo mengine ya nchi," amesema Waziri wa mambo ya Ndani wa Gabon, Pachomius Moubelet-Boubeya.
Jumuiya ya kimataifa imetoa wito wa kukomeshwa kwa vurugu na kuanza upya zoezi la uhesabuji wa kura za uchaguzi wa tarehe 27 Agosti.RFI

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger