TRA

TRA

Tuesday, March 7, 2017

Katibu Mkuu wa UN yuko Somalia kujadili baa la njaa

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres yuko nchini Somalia kujadiliana na Rais mpya wa nchi hiyo Mohamed Abdullahi Mohamed kuhusu baa la njaa linaloikumba nchi hiyo. Guteress amewaambia wanahabri wakati wa safari yake kuelekea Mogadishu kuwa mzozo, ukame, mabadiliko ya hali ya hewa, magonjwa na kipindupindu vyote kwa pamoja ni hali ya kutisha. Katibu huyo mkuu wa Umoja wa Mataifa atakutana na rais huyo mpya wa Somalia katika eneo la uwanja wa ndege wa Mogadishu ambalo liko chini ya ulinzi mkali wa wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika na ambako kuna ofisi za Umoja wa Mataifa na mashirika ya kutoa misaada ya kibinadamu. Hiyo ndiyo ziara ya tatu kufanywa na Katibu wa Umoja wa Mataifa Somalia tangu mwaka 1993, miaka miwili baada ya Rais Siad Barre kupinduliwa madarakani na kulitumbukiza taifa hilo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger