TRA

TRA

Tuesday, March 7, 2017

Wakuu wa jeshi la Uturuki, Marekani na Urusi wakutana

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Mkuu wa majeshi ya Uturuki anakutana na wenzake wa Marekani na Urusi katika mkoa wa kusini mwa Uturuki wa Antalya ili kujadili kuhusu usalama wa kikanda, hasa nchini Syria na Iraq. Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa kuhusu mkutano huo unaoandaliwa na Jenerali Hulusi Akar. Mwezi Agosti, wanajeshi wanaoongozwa na Uturuki walianzisha operesheni ya kulifurusha kundi linalojiita Dola la Kiislamu kutoka mpaka wa Uturuki na Syria na kuwazuia wapiganaji wa Kikurdi wa YPG kulikamata eneo hilo. Tangu walipowaondoa wapiganaji hao katika ngome yao ya al-Bab, mapigano yamelenga vijiji vya magharibi mwa Manbij, yakiwakutanisha waasi wanaoungwa mkono na Uturuki na Baraza la Kijeshi la Manbij, ambalo ni sehemu ya wanajeshi wanaoungwa mkono na Marekani wa Syrian Democratic Forces - SDF na ambao wanajumuisha kundi la YPG. Uturuki inaliona kundi la YPG kuwa sehemu ya chama cha wafanyakazi wa Kikurdi - PKK ambacho kinaendesha uasi nchini Uturuki

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger