TRA

TRA

Tuesday, April 25, 2017

Askofu Mkuu Marek ateuliwa Balozi wa Vatikani nchini Tanzania

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


BABA Mtakatifu Fransisko amemteua Askofu Mkuu Marek Solczyński kuwa Balozi mpya wa Vatikani nchini Tanzania. Kabla ya uteuzi huu, Askofu Mkuu Solczyński alikuwa Balozi wa Vatikani nchini Georgia, Armenia na Azerbaijan.

Itakumbukwa kwamba, Askofu Mkuu Solczyński alizaliwa Aprili 7, 1961 huko Stawiszyn, nchini Poland. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, mnamo Mei 28, 1987 akapewa Daraja Takatifu ya Upadri.


Baada ya kufanya utume wake katika masuala ya diplomasia sehemu mbali mbali, tarehe 26 Novemba 2011, Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI akamteuwa kuwa Askofu Mkuu na kumwekwa wakfu tarehe 6 Januari 2012. Askofu mkuu Marek Solczyński ameshiriki kikamilifu katika maandalizi ya hija ya kitume ya Baba Mtakatifu Fransisko nchini Georgia, Armenia na Azerbaijan aliyoitekeleza mwaka 2016.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger