Kombora la kinyuklia likiwa limebebwa na gari la kijeshi |
NA K-VIS BLOG NA MASHIRIKA YA HABARI, SEOUL/BEIJING/RUSSIA
WIZARA
ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ikisema Jeshi la Wananchi wa
Korea Kaskazini, (KPA), litajibiza kwa nguvu kubwa uvamizi wowote utakaofanywa
na Marekani.
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim |
"Kwa
sasa tumeweka nguvu za kinyuklia kujilinda wenyewe kutokana na vitisho vya
silaha za kinyuklia za Marekani. Tutajibu bila kusita hata kidogo na tutajibu
vita kwa vita, nyuklia kwa mtindo wetu wa mashambulizi ya kinyuklia na tuna
hakika tutaibuka washindi mwisho wa mapambano yetu na Marekani.” Taarifa hiyo
ilisema.
Korea
Kaskazini inatarajiwa kuadhimisha miaka 85 ya kuanzishwa kwa misingi ya Jeshi
la Wananchi wa Korea, (KPA), Jumanne Aprili 25, 2017, ambapo maadhimisho hayo
yanakamilisha mazoezi ya kijeshi wakati wa majira ya baridi. Wakati huo huo
Marekani na Korea Kusini, wanaendelea kufanya mazoezi ya pamoja yataendelea
hadi mwishoni mwa mwezi huu wa Aprili. Msemaji wa Wizara ya Muungano Muungano
wa Serikali ya Seoul, Lee Duk-haeng, amesema.
“Ni
hali ya kutapakaa kwa mazoezi ya vifaa vya kijeshi Korea Kaskazini na
maandalizi ya kimkakati ya vifaa hivyo imeelekezwa kwenye Rasi ya Korea (Korean
Peninsula), kwa sababu ya mazoezi ya kijeshi ya pamoja ya Korea Kusini na
Marekani.” Alisema Lee.
Manowari ya kubeba ndege ya Marekani US Carl Vinson |
Kwa
haraka haraka vita hii itayavutia au kuyahusisha mataifa sita, kwa upande
mmoja, Marekani ina washirika wake ambao ni Korea Kaskazini, na Japan, ambao
wote ni majirani na Korea Kaskazini, huku kwa upande mwingine, Korea Kaskazini
inaungwa mkono na China na Russia.
Naye
Rais wa Marekani amlisema Alhamisi iliyopita kuwa “mienendo isiyo ya kawaida
imekuwa ikijionyesha katika masaa mawili au matatu. Alisema anaimani na Rais wa
China Xi Jinping “atajaribu kwa nguvu kubwa” kuwashinikiza Korea Kaskazini
kuhusu nyuklia na mipango yake ya makombora.
Rais Trump na Rais Xi |
Hat
hivyo Trump hakuonyesha mienendo hiyo ina maanisha nini, na hakuna afisa yeyote
wa Marekani aliyeliambia Sirika la Habari la Uingereza Reuters, kuhusu kupanda
kwa joto la harakati za kijeshi za Makombora ya China yakiashiria kuwa wanajua
kwa usahihi sababu za miendendo hiyo.
Rais
Trump aliandika kwenye Tweeter yake kuwa “China ni msaidizi mkuu wa kiuchumi wa
Korea Kaskazini, wakati kutokuwa na kitu si rahisi, kama wanataka kutatua suala
la Korea Kaskazini wanaweza.” Aliandika.
Wizara
ya Ulinzi ya China imesema, majeshi yake yaliyoko kwenye mpaka wake na Korea
Kaskazini, yalikuwa yanajiimarisha katika hali ya kawaida ya kujiweka tayari
kijeshi na mafunzo.
Alipotakiwa
kuzungumzia tweet hiyo ya Trump, Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China, Lu
Kang alisema, Rais Xi na Trump walikuwa na majadiliano mapana kuhusu Korea
Kaskazini, walipokutana mwezi nchini Marekani.
Fukuto
la kutokea kwa vita kwenye Rasi ya Korea, linazidi kushika kasi huku Korea
Kusini ikisogeza vifaa vyake vya kijeshi kwenye kona zote za mpaka wake na
Korea Kaskazini Ijumaa Aprili 21, 2017.
Tayari
Marekani ambayo inatajwa kuwa ndiyo kinara wa “vita” hiyo, imekwisha sogeza
meli yake ya kubeba ndege, Carl Vinson kwenye Rasi ya Korea.
Joto
hilo la vita litazidi kupanda zaidi, Aprili 25, ambapo Pyongyang inatarajiwa
kufanya sherehe kubwa zaidi ya kijeshi ambapo tayari Korea Kaskazini imetishia
kufanya jaribio linguine la Kinyuklia.
“Tunafuatilia kwa karibu hali ya mambo,
alisema na kuongea Korea Kusini haiwezi kuacha ulinzi wake ukianguka.
Korea
Kaskazini imesema Ijumaa kuwa hali ni tete na hatari kwenye Rasi ya Korea kwa
sababu ya upuuzi (madcap) wa Marekani wa kutumia vita vya Kinyuklia kwa lengo
la kuingilia utawala wan chi hiyo na haki ya kuishi.”
Hali
ilizii kuwa tete kwenye miezi ya hivi karibuni baada ya Korea Kaskazini kufanya
majaribio mawili ya makombora ya kinyuklia mwaka jana na kufanya jaribio lingine
la kombora la masafa marefu, (Intercontinental ballistic missile).
Rais
wa Marekani, Donald Trump ameapa kuizuia Korea Kaskazini kuwa na uwezo wa
kuipiga Marekani kwa bomu la nyuklia.
Kaimu
Rais wa Korea Kusini, President Hwang Kyo-ahn amewaambia maafisa wa juu wa
serikali yake kuwa kuna shaka maadhimisho ya miaka 85 ya misingi ya jeshi la
Korea Kaskazini hapo Aprili 25, yakatumika kufanya uchokozi tena.
Vifaru vya Korea Kusini |
Picha
mpya za Satalaiti zinazochambua 38North, mradi wa kuratibu masuala ya Korea
Kaskazini wenye makazi yake mjini Washington Marekani umeona harakati za
kijeshi zikiendelea huko Korea Kaskazini kwenye eneo la kufanya majaribio ya
kinyuklia la Punggye-ri. Lakini wachambuzi hao hawaksuema kama harakati hizo
kuelekea jaribio linguine.
“Kando
na picha hizo za satalaiti kuendelea kuonyesha harakati hizo za kijeshi,
inaonyesha kuwa eneo hilo la Pungyang-ri, huenda likatumika kufanya jaribio la
sita la kombora la inyuklia.” 38North imesema katika uchambuzi wake Ijumaa
Aprili 21, 2017.
Maafisa
wa Marekani pia wamesema, kumekuwepo na hali isiyo ya kawaida kwa Wafyatua
makombora wa China hali inayoashiria kujiweka tayari kufuatia mshirika wake
mkubwa aliyetengwa, Korea Kaskazini kuzongwa na matishio ya vita. Hata hivyo maafisa
wa China wamepuuzia taarifa hizo na kukanusha taarifa kuwa ndege zake za
kijeshi zimewekwa tayari.
Jeshi
la Russia nalo limekanusha taarifa za vyombo vya habari Ijumaa iliyopita kuwa
lilikuwa likiviandaa vikosi vyake kwenye mpaka wake na Korea Kaskazini, Shirika
la habari la Ruassia Interfax limesema, likimnukuu msemaji wa jeshi la Russia.
Hwang Kyo-ah(kulia) na Tillerson |
“Moscow
imesema, mienendo ya kijeshi inayoonwa na wananchi kwenye maeneo hayo ni ya
kawaida na ilkuwa imepanwga kabla ya sekeseke la sasa.”
Habari
za hivi punde zinasema Korea Kusini imetangaza kuwa raia wa Marekani ametiwa mbaroni na maafisa wa
usalama wa Korea Kaskazini, kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Pyongrang Aprili 23, 2017.
Huyu
ni mtu wa tatu kutoka Marekani kukamatwa na maafisa wa serikali wa Korea.
Mmarekani
huyo mwenye asili ya Korea Kaskazini alikuwa anajiandaa kupanda ndege kurejea
Marekani, na kwamba alikuwa nchini humo kujadili masuala ya misada.
SHARE
No comments:
Post a Comment