TRA

TRA

Thursday, April 13, 2017

POLISI WATANO WAUAWA HUKO KIBITI MKOANI PWANI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !




NA K-VIS BLOG
POLISI wanaokadiriwa kuwa watano wameuawa katika shambulio la kuvizia wilayani Kibiti mkoa wa Pwani, Aprili 13, 2017.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amethubitisha kutokea kwa tukio hilo lakini hakutaja idadi kamili ya askari polisi waliouawa.
“Ni kweli askari wetu wanaokadiriwa kuwa watano, wakiwa katika gari lao la doria, wakitoka eneo la Jaribu Mpakani kurejea Kibiti walishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana na gari lao likapinduka lakini bado sijapata idadi kamili ya waliouawa.” Alisema.
Waziri Nchemba alisema, kimsingi shambulio hilo wanalichukulia kama ni kulipiza kisasi kwa wahalifu hao dhidi ya askari polisi ambao wamekuwa wakifanya kazi nzuri ya kuwadhibiti wahalifu hao ambao kwa sasa wanatafuta mahala pa "kujificha" mkoani Pwani baada ya kufurushwa jijini Dar es Salaam.
Waziri amesikitishwa na shambulio hilo na kuwataka Watanzania kuwa watulivu wakati jeshi la polisi linaendelea na operesheni ya kuwasaka wahalifu hao ambapo aliongeza kuwa taarifa kamili ya tukio hilo baya, itatolewa na Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani leo Aprili 14, 2017.
Kumekuwa na matukio ya polisi na watumishi wa serikali kushambuliwa na wahalifu mkoani Pwani ambapo tukio la hivi karibuni kabisa, polisi walimuua mwanamume mmoja aliyejaribu kuwatoroka polisi akiwa amevalia vazi la hijab linalovaliwa na wanawake.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger