TRA

TRA

Wednesday, April 26, 2017

SERENGETI BOYS YAIBUTUA TENA GABON 2-1 MCHEZO WA KIMATAIFA NCHINI MOROCCO

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !




Timu ya soka ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys imedhihirisha ubabe wake kwa wenyeji wa fainali za U-17 Afrika mwaka huu, Gabon baada ya kuwafunga tena 2-1 katika mchezo wa kirafiki mjini Rabat.
Mabao ya Serengeti Boys yamefungwa na Assad Juma na Abdul Hussein na hicho kinakuwa kipigo cha pili mfululizo vijana wa Tanzania wanawapa wavulana w Gabon, baada ya Aprili 22 kuwafunga pia 2-1, mabao ya Kelvin Nashon Naftali dakika ya 18 na Ibrahim Abdallah Ally dakika ya 75.
Serengeti Boys imeweka kambi ya mwezi mmoja nchini Morocco kujiandaa na Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17, zinazotarajiwa kuanza Mei 14 hadi 28, mwaka huu nchini Gabon.
Kwa ujumla huo unakuwa mchezo wa tano wa maandalizi kwa Serengeti kujiandaa fainali za Gabon, baada ya awali kuifunga Burundi mara mbili, Machi 30 mabao 3-0 na Aprili 1 mabao 2-0, mechi zote mbili zikipigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, kabla ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Ghana ‘Black Starlets’ Aprili 3 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Serengeti Boys itakuwa kambini mjini Rabat hadi Mei 1, mwaka huu itakapowenda Younde, Cameroon kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya wenyeji Mei 3 na 6, mwaka huu.
Mei 7 timu hiyo itakwenda Gabon ambako imepangwa kundi B pamoja na timu za Mali, Niger na Angola, wakati Kundi A lina timu za wenyeji, Gabon, Guinea, Cameroon na Ghana.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger