TRA

TRA

Wednesday, May 31, 2017

Wenger ashauriwa kuwauza Sanchez na Ozil

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Mlinzi wa zamani wa klabu ya Arsenal Martin Keown amesema kuwa meneja wa Klabu hiyo Arsene Wenger anapaswa kuwauza nyota wake Alexis Sanchez na Mesut Ozil baada ya kuongeza muda wa kusalia kinoa miamba hiyo ya London.

Mfaransa huyo amesaini mkataba wa miaka miwili na amesema kuwa timu yake inaweza kupigana na kutwaa ubingwa msimu ujao.
Viungo Alexis Sanchez na Mesut Ozil kwa pamoja wanamaliza mikataba yao mwishoni mwa mwaka huu.


 Kwa pamoja Sanchez na Ozil wamekuwa nguzo muhimu kwa klabu ya Arsenal

Kewon anasema kuliko kupata hasara ya kuwaruhusu kuondoka bure ni vyema akafanya maamuzi magumu ya kuwauza nyota hao na kutengeneza faida itakayoweza kuleta wachezaji wapya na wenye morali kubwa zaidi. 

Sanchez amefunga magoli 24 na kuchangia kupatikana kwa mengine 10 huku Ozil akifunga nane na kuchangia tisa lakini hiyo haikutosha kuifanya timu hiyo kukosa michuano ya mabingwa wa Ulaya msimu ujao jambo ambalo linatia ukakasi kwa Sanchez na Ozil kuongeza mikataba yao.

Sanchez amepewa ofa ya paundi 300,000 kwa wiki lakini bado hajasaini mkataba huo, huku Ozil akikataa paundi 250,000 kwa wiki.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger