TRA

TRA

Tuesday, June 20, 2017

Joto lasababisha safari za ndege kufutwa Marekani

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Huku joto likizidi kupanda katika mji wa Phoenix jimbo la Arizona nchini Marekani, zaidi ya safari za ndege 40 zimefutwa kwa sababu joto ni jingi kwa ndege kuruka.

Utabiri wa hali ya hewa katika mji huo unasema kuwa viwango vya joto katika mji huo vinaweza kufika nyuzi joto 120F au 49C siku ya Jumanne.
Hivyo ni viwango vya juu zaidi kwa ndege zingine kuweza kuruka.
Shirika la American Airlines, lilitangaza kuwa lilikuwa likifuta safari kadhaa zilizokuwa zitoke uwanja wa Sky Harbor.

 Shirika la American Airlines, lilitangaza kuwa lilikuwa likifuta safari kadhaa zilizokuwa zitoke uwanja wa Sky Harbor.
 
Taarifa kutoka Phoenix zilisema kuwa hatua hiyo iliathiri ndege ndogo ambazo viwango vya juu zaidi kuhudumu ni nyuzi 118F au 48C. 
Wakati wa viwango vya juu vya joto, hewa huwa nyepesi hatua ambayo husababisha kuwepo ugumu wa ndege kupaa kuenda mbali.
Kufuatia hilo ina maana kuwa ndege itahitaji nguvu nyingi zaidi kuweza kupaa angani.
Ndege kubwa kama ya Boeng 747 na Airbus zina uwezo wa kuhudumu katika viwango vya juu vya joto na hivyo hazijaathiriwa na viwango vya joto huko Phoenix.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger