TRA

TRA

Wednesday, July 19, 2017

Kipindupindu Kenya, hoteli zafungwa

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
Hoteli mbili zimefungwa mjini Nairobi kutokana na mlipuko wa ugonjwa kipindupindu mjini humo. 

Wizara ya afya ilitoa amri ya kufungwa hoteli hizo kufuatia watu kadha wakiwemo mawaziri wawili kulazwa hospitalini, baada ya kula chakula kilichokuwa kimepikwa na hoteli hizo mbili.
 Jiji la Nairobi

Watu wanne tayari wamefariki kutoka na ugonjwa wa kipindupindu tangu mwezi Mei na zaidi ya visa 300 vya ugonjwa huo vimeripotiwa.
Waziri wa afya Dr. Cleopa Mailu anasema hoteli hizo mbili zitasalia zimefungwa hadi zitimize viwango vipya vya wizara ya afya.

Wizara ya afya pia ilifuta leseni za sehemu zote za kupika chakula kote nchini, na kubuni jopo litakaloongoza hatua za serikali dhidi ya ugonjwa huo.

Vituo sita vya kutoa matibabu vimebuniwa hasa maeneo ya mabanda mjini Nairobi kuzuia kusambaa kwa ugonjwa wa kipindupindu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger