TRA

TRA

Thursday, July 20, 2017

MAVUNDE AWA GUMZO HOSPITAL YA RUFAA MKOA WA DODOMA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akisalimiana na wauguzi katika hospitali ya Rufaa ya Dodoma wakati wa uzinduzi wa matumizi ya mfumo wa Biometrics na kamera za CCTV katika Hospitali hiyo.



NA K-VIS BLOG, DODOMA
MBUNGE wa Dodoma mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, ((sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe.Anthony Mavunde ameendelea  kutatua kero katika sekta ya Afya jimboni humo ambapo leo Julai 20, 2017 amezindua matumizi ya mfumo wa Biometrics na kamera za CCTV katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma,kufuatia hali hiyo wagonjwa wengi waliokuwepo hospital hapo walionekana wenye furaha na kuunga mkono jitihada za mbunge wao katika kusaidia kuboresha huduma za Afya katika hospital hiyo.
Akizungumza katika uzinduzi wa matumizi ya vifaa hivyo, Mavunde amesema ufungaji wa mifumo hiyo ni miongoni mwa jitihada zake za kuhakikisha huduma za afya katika jimbo hilo zinatolewa ipasavyo.
Mavunde ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Ajira na Vijana amesema mfumo huo umefungwa na Ofisi ya Mbunge wa Dodoma na amelazimika kufunga vifaa hivyo kutokana na malalamiko ya muda mrefu ya wagonjwa kuwa wamekuwa wakitolewa lugha chafu na wauguzi.
Amesema pamoja na kamera hizo, pia umefungwa mfumo wa Biometrics(uchukuaji alama za dole gumba) ili kudhibiti  watumishi ambao wamekuwa wakiondoka kabla ya muda na kuchelewa kuingia kazini.
“Kamera hizi zinarekodi sauti na kuchukua video ili kuondokana na malalamiko yaliyotolewa na wananchi na itakuwa ni rahisi kumbaini mtu atakayelalamikiwa na mgonjwa,”amesema Mavunde
Mavunde amesema fedha alizotumia kununulia Kamera hizo na mfumo wa Biometrics amezipata kwa kujibana katika mshahara wake lengo likiwa ni kutekeleza ahadi yake aliyowaahidi wananchi wakati wa Kampeni kutatua kero za afya.
Aidha amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa wananchi hasa ukizingatia kwasasa Dodoma kuna ongezeko la watu kutokana na serikali kuhamia mkoani humo.
“Baadaye pia tutaweka mfumo wa kuhifadhi mafaili, hii yote ni kurahisisha utendaji kazi katika hospitali hii ili wananchi wetu waweze kupata huduma za afya ipasavyo.pia nimeomba vifaa mbalimbali vya kisasa Ujerumani kwa ajili ya hospitali hii tukipatiwa itasaidia sana utoaji huduma za afya,”amesisitiza Mavunde
Amesema ameahidi kutatua changamoto katika sekta ya afya ambapo mbali na ufungaji vifaa hivyo alishakabidhi vitanda katika Zahanati na Vituo vya afya 35.
“Nimetoa madawa kwenye kituo cha afya cha Makole yenye thamani ya Sh. Milioni 15,nimefunga umeme wa jua katika vituo vya Afya 17 pamoja na huduma za macho kwa watu 7000 na watu 3000 walipata huduma za upasuaji bure,”amesema
Naye, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,Dk.Caroline Damiani amemshukuru Mbunge huyo huku akidai kuwa matunda ya ufungaji wa kamera yameanza kuonekana kwa watumishi kufanya kazi zao kwa ufanisi wa hali ya juu tofauti na awali.
“Kumekuwa na kero nyingi kutoka kwa wagonjwa sasa Kamera za CCTV zitatusaidia kutatua kero hizi na kudhibiti wale wanaotoka kabla ya muda wa kazi kuisha au kuchelewa kazini,”amesema Mganga huyo
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufundi wa Kampuni ya Entersoft Limited,Keneth Yindi amesema wamefunga Kamera 4 pamoja na mfumo wa Biometrics  katika hospitali hiyo na ina uwezo wa kurekodi matukio kwa miezi tisa mfululizo.


Mkurugenzi wa Ufundi wa Kampuni ya Entersoft Limited,Keneth Yindi akitoa maelezo kuhusu matumizi ya kamera za CCTV na mfumo wa Biometrics katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma


Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa matumizi ya kamera za CCTV na Mfumo wa Biometrics katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma.


Mkurugenzi wa Ufundi wa Kampuni ya Entersoft Limited,Keneth Yindi akitoa maelezo kuhusu matumizi ya kamera za CCTV na mfumo wa Biometrics katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma kwa Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde.


Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akiangalia komputa  inayohifadhi video vinazorekediwa kwenye kamera za CCTV katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma.


Mkurugenzi wa Ufundi wa Kampuni ya Entersoft Limited,Keneth Yindi akitoa maelezo kuhusu matumizi ya kamera za CCTV na mfumo wa Biometrics katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma


Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizindua matumizi ya mfumo wa Biometrics katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger