Kama
ulikuwa una ndoto za kufanya kazi nchini Uganda hasa kwa watoto wa kike
wenye kupenda kujipodoa na kuvaa nguo zinazoonyesha maumbile basi jua
hautaweza kudumu wala kupata kazi nchini humo.
Hii ni
kutokana na sheria mpya iliyopo, Kwa mujibu wa mtandao wa edaily wa
Kenya, umeripoti kuwa serikali ya Uganda imepiga marufuku uvaaji wa nguo
fupi makazini, upakaji make up uliozidi, kubandika kucha ndefu na
bandia, kuweka nywele bandia na kuzipaka rangi, kuvaa nguo inayobana
kama vile Tshirt na magauni pamoja na kuvaa vivalio.
Miaka 2013 nchi hiyo ilitunga sheria ya kukataza kuvaa nguo fupi, sheria ambayo ilizua mijadala nchini humo na sehemu zingine.
SHARE
No comments:
Post a Comment