Wanajeshi 10
hawajulikani waliko na wengine watano wamejeruhiwa baada ya manowari
ya jeshi la Marekani kugongana na meli ya kubeba mafuta pwani mwa
Singapore, kwa mujibu wa jeshi la wanamaji la Marekani.
Shughuli kubwa ya kuwatafuta na kuwaokoa wanajeshi inaendelea.
- Wanajeshi wa Marekani waliokuwa na meli kuadhibiwa
- Meli ya Japan kuisindikiza meli ya Marekani
- Iran yatimua meli ya Marekani
Manowari ya Marekani yagongana na meli ya mafuta pwani mwa Singapore
Ripoti zinasema kuwa manowari hiyo ilikumbwa na uharibifu upande wake mmoja, lakini jeshi la Marekani lilsema kwa inaelea peke yake kwenda bandari ya Singapore.
Helikopta za jeshi la Marekani na jeshi la Singapore pamoja na walinzi wa pwani, wanafanya shughuli za uokoaji. Malaysia nayo imejiunga katika shughuli hiyo.
Kura taarifa kidogo kuhusu hali ya meli ya mafuta ya Alnic MC na wahudumu wake.
Meli hiyo ya mafuta inaripotiwa kuwa na uzito mara tatu wa manowari ya jeshi ya USS John McCain, na taarifa zinasema kuwa haikuwa imebeba mafuta wakati ya ajali hiyo.
Seneta John McCain ambaye jina lake limepewa manowari hiyo, aliandika kwenye mtandao wa twitter kuwa yeye na mke wake wanawaombea mabaharia hao.
Mwezi Juni mabaharia saba wa Marekani waliuawa wakati manowari ya USS Fitzgerald iligongana na meli ya mizigo kwenye bahari ya Japan karibu na bandari ya Yokosuka.
CHANZO: BBC
SHARE









No comments:
Post a Comment