
Mwenyekitiwa Chama cha Wanawake katika Utalii Tanzania (AWOTTA),Mary Kalikawe (katikati) akisisitiza jambo kwa wanachama (hawapo pichani) wakati wa mkutano mkuu wa mwaka ulioambatana na sherehe za kutimiza miaka sita ya chama hicho zilizofanyi jijini Dar es Slaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Devotha Mdachi na Katibu wa chama hicho, Agnes Rwegasira .

Katibu Mkuu wa Chama cha Wanawake katika Utalii Tanzania (AWOTTA) , Agnes Rwegasira akisisitiza jambo kwenye semina hiyo. iliyofanyika katika ofisi za Bodi ya Utalii Tanzania ( TTB) jijini Dar es Salaam

Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Utalii (TTB) Bi. Fatma s. Mchumo(kushoto) akitoa mchango kwenye semina hiyo

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Wanawake nchini Tanzania Bi. Jacqueline Maleko. (TWCC ) kulia, akiongea wakati wa semina hiyo

Mkuu
wa idara , Sera na Mpingo wa Wizara ya Maliasili naUtalii Tanzania,
Dorothea Masawe (katikati) Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake katika
Utalii Tanzania (AWOTTA) Mary Kalikawe (wapilikushoto) na Mkurugenzi
Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Devotha Mdachi (wa tatu kutoka kulia) wakikata keki ya kuadhimisha miaka 6 ya AWOTTA.

Baadhi ya wanachama na wafanyakazi wa chama cha Chama cha Wanawake katika Utalii Tanzania (AWOTTA) wakiwa kwenye mkutano Mkuu wa Mwaka uliaoambatana na sherehe za kutimiza miaka sita tangu kuanzishwa kwa chama hicho. Wakati wa hafla na semina iliyofanyika katika ofisi za TTB jijini Dar es salaam
………………………….
Wakati
serikali ya awamu ya tano imejipanga kuipeleka Tanzania katika uchumi
wa kati na kuimarisha zaidi sekta ya viwanda,Wanawake wanaojishughulisha
na utalii kupitia umoja wao unaojulikana kama Association of Women in
Tourism Tanzania (AWOTTA) umeweka mikakati mikubwa ya kuhakikisha inatumia fursa zilizopo kukuza sekta ya utalii.
Akiongea wakati wa mkutano wa mkuu
wa mwaka, hafla ya kuadhimisha miaka 6 ya umoja huo sambamba na semina
ya kujadili changamoto na kuweka mikakati iliyofanyika jijini Dar es
Salaam,Mwenyekiti wa AWOTTA,Mary Kalikawe,aliipongeza serikali ya awamu
ya tano chini ya uongozi wa Rais,Dk.John Magufuli,kwa jitihada
inazofanya kukuza uchumi kwa nchi kupitia sekta mbalimbali.
Kalikawe
alisema kuwa katika kipindi cha miaka 6 tangu ianzishwe AWOTTA
imefanikiwa kwa kuwaunganisha wanawake wanaofanya biashara ya utalii
hapa nchini kwa upande wa bara na visiwani na aliwataka akina wanawake
wengi kujitokeza kujiunga na umoja huu kwa kuwa umoja ni nguvu katika
kukabiliana na changamoto mbalimbali kisekta.
Alibainisha baadhi
ya changamoto zinazokwamisha wanawake kuendesha shughuli za utalii ni
kutokuwa na mitaji ya kutosha,kodi nyingi na kubwa zinazotozwa na
serikali katika sekta
hiyo,na wananchi na wadau wengi kutokuwa na ufahamu kuhusiana na sekta
hii japokuwa inachangia pato la taifa kwa kiasi kikubwa na aliiomba
serikali kusaidia kukabiliana na changamoto hizo hili sera ya Tanzania
ya viwanda iende sambamba na fursa za kukuza utalii nchini.
Kwa
upande wake,Afisa Mwandamizi kutoka kitengo cha sera na Mipango,
Dorothea Masawe ambaye alimwakilisha Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili
na Utalii,Mh.Ramo Makani katika maadhimisho hayo aliipongeza AWOTTA kwa
kazi nzuri inayofanya ya kuunga mkono jitihada za serikali za kukuza
sekta ya utalii na aliahidi kuwa serikali itafanya kazi kwa kushirikiana
na taasisi hiyo “Serikali inatambua kazi nzuri inayofanywa na AWOTTA
katika kukuza utalii nchini,inawapongeza kwa kutimiza miaka 6 na
itaendelea kufanya kazi nanyi bega kwa bega”.Alisisitiza.
SHARE








No comments:
Post a Comment