TRA

TRA

Monday, September 4, 2017

POLISI WAPEWA ONYO RPC SHANNA AWAKALIA MGUU KAUSHA ASKARI WALA RUSHWA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



SAM_5288
Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP)Jonathan Shanna ,wa katikati akizungumza na askari mbalimbali wa mkoani hapo .(picha na Mwamvua Mwinyi )
……………………………………………………………
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
JESHI la polisi mkoani Pwani , limetoa onyo kwa askari wa vitengo mbalimbali mkoani hapo ,kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa na atakabainika atachukulia hatua kali za kijeshi.
 Aidha jeshi hilo ,limejipanga ipasavyo kwa kutumia askari waliopo katika kila himaya ili kupambana na uhalifu kwa kuweka mikakati ambayo itakua ni muongozo na dira kwenye utendaji kazi wake .
Akizungumzia suala la rushwa kwa askari,kamanda wa polisi mkoa wa Pwani (ACP)Jonathan Shanna,aliwataka wanaohusika na chumba cha mashitaka,upelelezi mdogo,kitengo cha upelelezi na usalama barabarani wasiruhusu mianya hiyo .
Aliwaagiza kuhakikisha majalada ya kesi yanafikishwa mahakamani na wapepelezi wa kesi hizo kuzisimamia ipasavyo kwa kuwa jeshi la polisi ni chombo cha kisheria.
Kamanda Shanna ,alieleza hatakuwa na muhali kwa watendaji watakaobainika kujihusisha na vitendo vya kushawishi,kuomba na kupokea rushwa kutoka kwa watuhumiwa ama walalamikaji.
“Kuipa rushwa nafasi ni kuruhusu kushindwa kupatikana kwa haki kwa anaekusudiwa kuipata haki hiyo kisheria “
“Askari wawajibike ili kuondoa mapungufu katika utendaji kazi ,wananchi wanategemea huduma iliyo bora kutoka jeshi letu ,alisisitiza.
” Sitomvumilia askari atakayekiuka maelekezo haya ,kila mmoja anatambua wajibu na mipaka yake ,sitategemea kupata malalamiko kutoka ndani ya jamii kufuatia utendaji mbovu wa askari wangu “alisema kamanda Shanna.
Kamanda Shanna aliwaomba  wananchi watoe ushirikiano kwa viongozi wa jeshi la polisi na taasisi husika ya kupambana na vitendo vya rushwa (TAKUKURU )ili kuwafichua askari wote wanaofanya vitendo hivyo.
Hata hivyo ,alieleza katika kipindi cha uongozi wake ameelekeza kuanzia kwa maafisa ,wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali kufanyakazi kwa weledi na usasa ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kwa wakati .
Kwa mujibu wa kamanda Shanna ,anatambua mchango wa kila mmoja wao kwa nafasi yake kwenye jitihada za kukomesha vitendo vya uhalifu .
Alisema ana imani na utendaji kazi wa askari wote katika vikosi vyao ,uwezo wao na uwajibikaji wa kila siku kwani umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uhalifu .
Kamanda Shanna ,hakusita kutoa rai kwa wananchi kuzidi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kuwafichua wahalifu waliopo kwenye maeneo yao ili wachukuliwe hatua za kisheria .
Anasema kwa kufanya hivyo itawezesha kutokomeza uhalifu mkoani Pwani .

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger