TRA

TRA

Saturday, September 9, 2017

SAKATA LA LISSU LAMUIBUA GWAJIMA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


SeeBait
Askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima amefunguka na kusema kuwa siku ya Jumapili atafanya maombezi maalum kwa afya ya Mbunge Tundu Lissu ambaye juzi alipigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa Dodoma nyumbani kwake.
Askofu Gwajima amesema kuwa atatumia misa hiyo kulaani vikali kitendo cha kinyama alichofanyiwa Tundu Lissu na watu hao wasiojulikana ambao waliweza kupiga gari lake zaidi ya risasi 30 huku risasi tano ndizo ziliweza kumjeruhi Mbunge huyo.
"Jumapili hii Septemba 10, 2017 nitaongoza maombi maalumu ya kuombea Afya ya Mhe. Tundu Lissu na kulaani Vikali kitendo cha Kikatili na Kinyama alichofanyiwa. Maombi haya yatafanyika katika Kanisa la Ufufuo na Uzima, Ubungo Dar es Salaam tunawakaribisha wote watakaopenda kuungana nasi katika maombi haya" aliandika mchungaji Gwajima kupitia ukurasa wake wa facebook

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger