TRA

TRA

Saturday, September 9, 2017

TAARIFA MUHIMU YA VITAMBULISHO KWA WAZEE

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


nida_clip
USAJILI WA WAZEE WA WILAYA YA UBUNGO VITAMBULISHO VYA TAIFA
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), inapenda kuwajulisha wazee wote wa mkoa wa Dar-es-salaam Wilaya ya Ubungo kuwa, zoezi la Usajili na Utambuzi lenye lengo la kuwapatia Vitambulisho vya Taifa linaendelea sambamba na zoezi la Usajili wa Kadi za Bima ya Afya kwa wazee chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.
Wahusika ni wazee wote wanaoishi Wilaya ya Ubungo. Unachotakiwa kufanya ni kuchukua na kujaza fomu ya maombi ya  Usajili. Fomu zinapatikana ofisi ya Mtaa unakoishi au Ofisi ya Kata. Unapojaza fomu ya maombi unatakiwa kuweka na nakala ya  viambatisho muhimu vinavyokutambulisha vile ulivyonavyo mathalani Kadi ya Kupigia kura, Barua ya Serikali ya Mtaa, vyeti vya shule na kisha fika na fomu yako ikiwa imejazwa pamoja na vivuli (photocopy) ya viambatisho hivyo kwenye kituo cha karibu kusajiliwa.
Unapofika kusajiliwa unashauriwa kwa ajili ya ubora wa picha kutovaa nguo nyeupe, kijivu, bluu, pinki, au rangi yoyote inayoshabihiana na nyeupe, nguo zenye nembo, kofia aina yeyote ama kupaka hina kwenye viganja vya mikononi.
Kwa kuanza wiki ijayo Ratiba ya Usajili itakuwa ni kama ifuatavyo:-
Na KITUO CHA USAJILI MUDA TAREHE
1. Kata ya  Makurumla Saa 3:00 – 11:00 jioni 11/09/2017
2. Kata ya Manzese Saa 3:00 – 11:00 jioni 12/09/2017
3. Kata ya Sinza Saa 3:00 – 11:00 jioni 13/09/2017
4. Kata ya Makuburi Saa 3:00 – 11:00 jioni 14/09/2017
 Utaratibu wa Usajili katika Kata zingine tutaendelea kuwafahamisha. Kupata maelezo zaidi tafadhali wasiliana na mtendaji wako wa Mtaa au Mtendaji Kata.
 Kwa taarifa zaidi kuhusu Vitambulisho vya Taifa tembelea Tovuti yetu www.nida.go.tz au ukurasa wetu wa facebook -nidatanzania au twitter @nidatanzania
 Wazee jitokezeni kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa ili mtambulike na kupata huduma za kijamii kwa haraka na kwa uhakika zaidi.
 Limetolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger