Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akimkabidhi Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) katika Nchi za
Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, Bibi Mary Kawar kitabu baada
ya kuzindua Miongozo ya Mafunzo Katika Maeneo ya Kazi kwenye ukumbi wa
LAPF mjini Dodoma Septemba 16, 2017. Watatu kushoto ni Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana , Ajira na Wenye
Ulemavu, Jenista Mhagama na wapili kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara
na Uwekezaji, Charles Mwijage. Kulia ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi
na Tekinolojia, Mhandisi Stella Manyanya na kushoto ni Naibu Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony
Mavunde.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya washiriki wa uzinduzi
wa Miongozo ya Mafunzo Katika Maeneo ya Kazi uliofanywa na Waziri Mkuu
kwenye ukumbi wa LAPF mjini Dodoma Septemba 16, 2017.(Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Baadhi ya washiriki wa uzinduzi
wa Miongozo ya Mafunzo Katika Maeneo ya Kazi uliofanywa na Waziri Mkuu
kwenye ukumbi wa LAPF mjini Dodoma Septemba 16, 2017.(Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,
Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama baada ya kuzindua
Miongozo ya Mafunzo Mahala pa Kazi kwenye ukumbi wa LAPF mjini Dodoma
Septemba 16, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza wakati alipozindua Miongozo ya Mafunzo katika Maeneo ya
Kazi kwenye ukumbi wa LAPF mjini Dodoma Septemba 16, 2017. Kulia ni
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana,Ajira na
Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa Shirika
la Kazi Dunia wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanbda na Burundi, Mary
Kawar. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akiwa katika picha ya pamoja na viongozi walioshiriki katika Uzinduzi
wa Miongozo ya mafunzo Katika Maenneo ya Kazi alioufanya kwenye ukumbi
wa LAPF mjini Dodoma Septemba 16, 2017.(Picha na Ofisi ya Wziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akigana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,
Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama baada ya kuzindua
Miongozo ya Mafunzo Mahala pa Kazi kwenye ukumbi wa LAPF mjini Dodoma
Septemba 16, 2017. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji,
Charles Mwijage na kushoto ni Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu, Kazi,Vijana na Ajira, Anthony Mavunde. Watatu kulia ni Mkuu wa
Wlaya ya Kongwa, Deogratius, Ndejembi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
…………………………………………………………………
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amezindua miongozo ya Kitaifa ya Kusimamia Mafunzo ya Vitendo kwa
Wahitimu (Internship Guidelines) na Mafunzo ya Uanagenzi
(Apprenticeship Guidelines) mahala pa kazi, leo (Jumamosi, Septemba 16)
mjini Dodoma.
Amesema miongozo hiyo inalenga
kuongeza ari kwa waajiri na wadau wengine kushiriki katika kutoa
mafunzo ya kukuza ujuzi na stadi za kazi ili kuhakikisha wahitimu na
wanagenzi wanapata stadi za kazi na ujuzi stahiki wa kuajirika au
kujiajiri.
Waziri Mkuu amesema miongozo
hiyo ambayo inakwenda kuboresha mafunzo ya uanagenzi na kwa wahitimu
itachochea ukuzaji wa viwanda na kupunguza ukosefu wa ajira kwa
watanzania hususan vijana.
Amesema Serikali imekua ikipokea
malalamiko kutoka kwa waajiri kwamba wahitimu wengi wa ngazi mbalimbali
za mafunzo wanaingia katika soko la ajira wakiwa hawana ujuzi
unaohitajika na hivyo waajiri kulazimika kutafuta wafanyakazi kutoka nje
ya nchi.
Amesema baada ya kupokea
malalamiko hayo Serikali, Waajiri na Wafanyakazi na walikubaliana
kuimarisha mfumo wa utoaji mafunzo yanayofanyika maeneo ya kazi ili
kuhakikisha mafunzo yatolewayo maeneo ya kazi yana ubora unaohitajika.
“Kuimarisha uwezo wa nguvu kazi
ya Taifa ni muhimu na njia bora ni kuboresha utoaji mafunzo kwa vitendo
mahali pa kazi kwa kuweka miongozo bora itakayowaongoza wadau wote
wakiwemo Serikali, Waajiri, Wafanyakazi na Vijana kutoa Mafunzo.”
Waziri Mkuu amesema Rais Dkt.
John Magufuli alipoanza kuweka malengo ya ujenzi wa viwanda, mbali na
kuwezesha kukua kwa kilimo na kuongeza thamani mazao, pia alilenga
kupanua wigo wa ajira za viwandani ambapo kiwanda kinaweza kuajiri watu
zaidi ya 1000.
Amesema miongozo hiyo itasaidia
kuboresha mazingira ya biashara nchini kwa kuhakikisha Taifa linakuwa na
nguvu kazi yenye weledi wa kutosheleza mahitaji ya soko la ajira na
kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu,
Bi. Jenista Mhagama amesema miongozo hiyo inaweka mfumo madhubuti wa
kuandaa, kutekeleza, kusimamia, kuratibu na kufuatilia mafunzo husika
mahala pa kazi.
Pia miongozo hiyo inabainisha
majukumu ya wadau muhimu wa mafunzo hayo ambayo ni pamoja na kuweka
bayana utaratibu wa kugharamia mafunzo ikiwa ni pamoja na kushirikisha
Serikali, waajiri na wazazi.
“Miongozo imebainisha majukumu
ya wadau katika kutoa mafunzo ambao ni Serikali, waajiri, taasisi za
mafunzo, taasisi za mitaala na wanagenzi na wahitimu. Pia imebainisha
vigezo vya kuwapata washiriki wa mafunzo na muda wa mafunzo.”
Pia miongozo hiyo imebainisha mfumo wa kitaasisi wa kuratibu
na kuhakikisha ubora wa mafunzo kwa kuunda kamati ya Utatu wa Taifa ya
kuratibu, kufuatilia tathmini ya mafunzo chini ya usimamizi wa Ofisi ya
Waziri Mkuu.
SHARE
No comments:
Post a Comment